WAKULIMA, WAFUGAJI KITETO WANUSURIKA KUZICHAPA KWENYE MKUTANO


Wakulima,Wafugaji wanusurika kuzichapa Kiteto. 

·          Ni baada ya kutofautiana kauli kwenye mkutanoni
·         Polisi waingia mitini,wadai walitumia busara

NA.MOHAMED HAMAD MANYARA
Mkutano maalumu uliokuwa umeitishwa na baadhi ya vijana wa jamii ya Kifugaji Wilayani Kiteto kujadili mgogoro wa ardhi katika eneo la Emboley Murtangos umeingia dosari mjini Kibaya baada ya pande hizo kutofautiana kauli

Awali akizungumza kwenye mkutano huo mmoja wa wanajamii ya kifugaji Abel Mainge alisema lengo la mkutano huo ni kuleta maridhiano kati ya wakulima na wafugaji ambayo yalitoweka na kusababisha madhara mbalimbali yakiwemo maafa katika pande hizo

Wakati pande hizo zikitunishiana misuli Jeshi la Polisi Wilayani Kiteto lilishindwa kuingilia kati kutuliza mzuka wa wananchi uliodumu kwa zaidi ya saa moja na nusu hadi walipoamua kuachana wenyewe kwa kuvunjika mkutano huo maalumu

“Leo ni siku ya peke kufanya mkutano mkubwa bila kuwa na viongozi wetu, nia ni kutaka kuwekana sawa ili tuweze kuishi kwa amani kwani kila mara tumekuwa tukishuhudia maafa yanayotokana na kugombania ardhi”alisema Abel

Wakati hayo yakisemwa msafara wa madereva wa pikipiki almaarufu Bodaboda waliingia na ujumbe maalumu juu ya kilio chao cha kukataa kuondolewa watu walioitwa wavamizi kutoka wilaya na mikoa mbalimbali hapa nchini katika eneo la Emboley Murtangos

Ghafla hali ilibadilika badala ya madereva hao kuja na mabango ambayo hayakutarajiwa kwenye mkutano huo ambao uliokuwa na waandishi wa magazeti na Televisheni wakipika picha kwaajili ya kuripoti ktika vyombo vyao vya habaro juu ya matukio hilo

Baadhi ya mabango hayo yalisomeka kuwalaumu viongozi wa Wilaya, Mkoa, na Taifa kwa kushindwa kuingilia kati kutatua migogoro ya ardhi,Kutotambuliwa kwa eneo la Emboley Murtangos, pamoja na kulaani ubaguzi wa Kikabila unaofanywa na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Kiteto

Wakati hayo yanajitokeza Polisi walifika kwenye mkutano huo wakiwa na kamera zao za video na picha za mnato wakipiga picha malumbano kati ya pande hizo kabla ya kuanzwa kwa mkutanona kisha kutoweka kusiko julikana hadi vurugu zilipoisha

Hata hivyo RAI lililazimika kuzungumza na baadhi ya walinzi hao wa amani (Polisi) kuwa kwanini waliondoka kwenye mkutano huo kwakuwa ulikuwa na kibali chao na kusema hali haikuwa shwari na kwamba walilazimika kutumia busara kuondoka

“Mwandishi wakati mwingine Polisi tunalazimika kutumia busara katika masuala kama haya, tungeingilia kati tungezidisha mgogoro, tumelazimika kuondoka kidogo ili waelewane wenyewe jambo ambalo pande hizo ziliachana kwa kuondoka kwenye mkutano huo

Paulo Tunyoni mtumishi wa shirika la MWEDO,Michael Williamu Afisa habari wa Halamshauri ya Wilaya ya Kiteto,pamoja na Shukumu Tuke wa Shirika la CORDS na vijana wengine wa waliokuwa wameandaa mkutano huo walisikika wakisema walikuwa na nia njema kuunganisha wakulima na wafugaji badala yake imeshindikana

Kwa upande wao wakulima wakiwakilishwa na Bakari maunganya alisema kamwe hawawezi kuridhia kinachofanywa na wafugaji kwani wamekuwa wakiwasumbua kwa kuwafukuza katika maeneo yao kwa kushirikiana na Serikali wakidai kuwa wameanzisha hifadhi ya Msitu

Wakati hayo yakijitokeza baadhi ya vijana wamesikika wakimlaumu Mbunge wa Jimbo lao la Kiteto Benedict Ole Nangoro kuwa hawasaidii wanapopata matatizo kwa kuwa yuko mbali nao kwa kuishi Dar es Salaam Kishuhuli

Mbunge wa Jimbo la Kiteto ambae pia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi amekuwa akifanya shughuli zake Dar za Kiserikali na kwamba kukosemana kwake kumewafanya wananchi wakose mtu wa kumweleza matatizo yao

RAI limelazimika kuzungumza na na katibu wa Mbunge huyo Singo Ndoera na kusema matatizo ya wanakiteto hayamalizwi na mbunge kuwepo Jimboni bali na kuongeza kazi ya Mbunge sio kutatua migogoro ambayo ina vyombo vya utatuzi

Mwisho

Maoni