AIBU YA MWAKA KWA VIONGOZI KITETO


Wanafunzi 32 walala chini kwa miaka mitano mfululizo
  • ·       Ni kwa kukosa vitanda shuleni

Na. Mohamed Hamad KITETO
JUMLA ya wanafunzi wa kiume 32 wa shule ya msingi na ufundi Kibaya iliyoanzishwa mwaka 1950 Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, wanalazimika kulala chini kwa kukosa vitanda kwa zaidi ya miaka mitano mfululizo

Wakizungumza hayo wanafunzi wanaoishi shuleni hapo  wamesema kwa miaka mitano wamekuwa wakilala chini kwa kukosekana vitanda baada ya vile vilivyokuwa vikitumika kuchakaa

Wamesema mbali na matatizo hao yanayowakumba pia shule hiyo ina upungufu mkubwa wa samani na thamani hali inayosababisha usumbufu mkubwa wanapokuwa shuleni

Wamesema shule ina upungufu wa viti 39 vilivyopo 11, na meza 37 za waalimu zilizopo 13, vyumba vya madarasa 5 vilivyopo 8, nyumba za walimu 13 zilizopo 6 pamoja na matundu 23 ya vyoo kati ya 6 yaliyopo

Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule hiyo Bi.Msangi alieleza Gazeti hili kuwa shule inakusudiwa kufungwa kwa kukosa choo chenye hadhi hivyo kuhofiwa wanafunzi kudumbukia wanapoenda kujisaidia

Simon Parseko (mwanafunzi) aliwaomba wadau wa elimu wilayani Kiteto na na nje ya Wilaya kuwasaidia vitanda, magodoro na shuka kwani wamechoka kulala chini kwa zaidi ya miaka mitano


“Mwalimu alituambia tuwaeleze wazazi wetu watununulie vitanda ili tuje navyo hapa shuleni lakini ilishindikana kutokana na kutojua aina ya kitanda kinachohitajika hivyo kutulazimu kuendelea kulala chini”

Naye Bakari Mahanyu ambaye ni mmoja wa maafisa wa Elimu Wilayani hapo alitupia mpira Serkali ya Kijiji kuwa ndio wenye jukumu la kufanya ukarabati shuleni unapohitajika

Alisema Serikali imekwisha sogeza huduma karibu na wananchi hivyo wenye jukumu la kuendeleza shule ni pamoja na wadau wa Elimu, wazazi pamoja na Serikali ya Kijiji na si vinginevyo

Mwisho 

Maoni