MWALIMU MBORONI KWA KUJIHUSISHA KIMAPENZI NA WANAFUNZI



Mwalimu mbaroni kwa kujihusisha mapenzi na mwanafunzi

Na Mohamed Hamad
JESHI la Polisi Wilayani Kiteto Mkoani Manyara linamshikilia mwalimu Abubakar wa Kiteto Sekondari kwa tuhuma za kufanya mapenzi na mwanafunzi wakiwa nyumbani kwao usiku wa kuamkia julay 19 mwaka huu

Kwa mujibu wa taarifa za kipolisi uchunguzi wa tukio hilo unaendelea kwa mwanafunzi wa kike jina limehifadhiwa kuendelea kufanyiwa vipimo huku mahojiano kwa mtuhumiwa yakiendelea

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa siku hiyo mwalimu alifika nyumbani kwa mwanafunzi huyo majira ya usiku wa manane ambapo ndugu walimfumania kisha kumkamata na kumpeleka kituo cha polisi Kiteto

“Kwa kweli hata kama ni masomo hayakupaswa kufanywa nyakati hizo kwani ule ulikuwa ni muda wa kulala sanane za usiku, tunatarajia kuona sheria ikichukua mkondo wake lakini pia huo ni ukosefu wa maadili ya kitaaluma kwa mwalimu huyo”alisema mmoja wa mashuhuda

Hata hivyo MTANZANIA jumapili iliweza kumwona mwalimu huyo akifanyiwa mahojiano kituo cha polisi Kiteto juu ya tukio hilo ambapo kwa taarifa za awali imeelezwa kuwa baada ya ripoti ya Hospitali kupatikana hatua zaidi zitajulikana

Kwa upande wake John Kimaro mkuu wa shule ya Kiteto Sekondari alieleza kuwa amesikitishwa na kitendo hicho akisema tuhuma hizo zinachafua kada ya ualimu na kwamba anawaweka pabaya walimu wenzake

“Binafsi nililazimika kutoa taarifa hivi karibuni kwa mwajiri juu ya nyendo za mwalimu huyu nilitegemea hatua zingechukuliwa lakini hata hivyo nadhani kwa hili hata kama hahusiki ama anahusika lazima mwajiri aone kwa undani juu ya mwenendo wa mwalimu huyu”alisema Kimaro

Kwa upande wa familia ya mwanafunzi wameitaka Serikali kuchunguza suala hili kwa kina ili kutokomeza vitendo hivi na kama wataviachia madhara makubwa yanaweza kujitokeza siku za usoni kwa jamii kuamua kuchukua hatua badala ya kuiachia polisi

Nae mjumbe wa bodi Mashaka Saidi Fundi ambaye pia ni mwangalizi wa haki za binadamu Wilayani Kiteto amelitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi zake kwa uadilifu kuchunguza ili kubaini kilichotokea ili sheria iweze kufuata mkondo wake na kwamba vitendo kama hivyo viweze kutokomeza

Mwisho

Maoni