WAJAWAZITO KITETO WALALAMIKA HUDUMA MBOVU




Wajawazito Kiteto walalamika huduma mbovu

NA Mohamed Hamad MANYARA
AKINAMAMA wajawazito wilayani Kiteto mkoani Manyara wameingia katika malumbani na uongozi wa Hospitali  ya wilaya ya Kiteto baada ya kutozwa Tsh 30,000 wakati wa kujifungua

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  wamesema pamoja na kutozwa fedha hiyo hawapati risiti kuhalalisha malipo yao jambo ambalo linawapa hofu kuwa wanahujumiwa huku Serikali ikisema huduma hiyo ni bure

“Mama mjamzito akifika hospitali analazimika kutalipa kila kitu kuanzia kadi vipimo pamoja na vifaa vyote vinavyohitajika wakati Serikali imetangaza kuwa huduma hiyo ni bure hali inayoleta usumbufu”alisema mmoja wa akinamama hao

Alisema pamoja na kutolewa taarifa kwa viongozi wanao husika wa Hospitali hiyo huambulia kauli za kuwa “hiyo ndio Serikali yenu lazima mchangie na hakuna dawa za bure ”hivyo hali hiyo inatofautiana na kauli ya Serikali  kuwa huduma hiyo ni bure

Kwa upande wa uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Kiteto wakizungumzia sakata hili walisema kuna upungufu wa dawa katika Hospitali na kwamba ili kukabiliana na tatizo hilo wananchi wanatakiwa wajiunge na mfuko wa jamii CHF

“Swala hili linafahamika nchi nzima kwamba Serikali haina fedha pamoja na kupata dawa kutoka MSD bado tuna tatizo la kutokidhi dawa hizo kwa wananchi hii inatokana na wengi wao kuto jiunga na mfuko wa afya”alisema Dr Joseph Tutuba mganga mkuu wa hospitali hiyo

Aliwataka wananchi Wilayani humo kujiunga na mfuko huo ambao utakuwa na msaada mkubwa kwao na kwamba kila mtu aliyejiunga atapata huduma hiyo kwa wakati na pia dawa hazitakosekana

Mwisho

Maoni