WAKULIMA KITETO WAITAKA SERIKALI KUBORESHA MASOKO YA MAZAO YA KILIMO



Wakulima Kiteto wahofu kutouza mazao yao Serikalini

Na.Mohamed Hamad Kiteto
Hofu ya wakulima kutouza mazao yao imetanda wilayani Kiteto Mkoani Manyara baada ya Serikali kutangaza kuwa ina uwezo wa kununua tani elfu moja sawa na gunia elfu kumi huku kukiwa na hitaji kubwa la wakulima kutaka kuuza mazao yao

Serikali kupitia kitengo cha National Food Reserve Authority cha Dodoma (NRFA) imeamua kuweka kambi kijiji cha Engusero ya kununua mazao hayo aina ya mahindi kwa wakulima ili kuwapunguzia adha ya kulanguliwa

Hata hvyo gazeti hili lilifika kituoni hapo na kuongea na wakulima ambao walisema kuna changamoto katika zoezi hilo zikiwemo rushwa pamoja na utaratibu mbobu wa kupokea mazao hayo

Walisema Serikali kutangaza kununua tani elfu moja inasababisha kuwepo kwa hujma mbalimbali  hali inayofanya wakulima wadogo kushindwa kuuza mazao yao kwenye soko hilo hivyo kutekwa na wafanya biashara wakubwa

Kilo moja ya mahindi inanunuliwa kwa sh 500 tofauti na soko la Kibaigwa lililopo Kongwa  hivyo kufanya soko hilo kutekwa na wafanya biashara hao wakubwa kutoka ndani na nje ya wilaya ya Kiteto huku rushwa ikidaiwa kushamiri  

Kwa mujibu wa Diwani wa kata ya Engusero Leonard Kunamila amewahakikishia wakulima hao kuwa atapambana na urasimu huo na kwamba kila mmoja atauza mazao yake hadi hapo Serikali itakapositisha kununua mazao hayo

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Engusero Haji Bundala ameitaka Serikali kuongeza fedha ili kukidhi mahitaji ya wakulima  kuuza mazao yao kwa bei hiyo kwa kuwa imekuwa na tija kubwa hivyo wengi wao watanufaika

“Hapa tuna makundi mengi ya wakulima wapo waliokopa fedha benki kwaajili ya kufanya kazi ya kilimo ambapo sasa wanadaiwa na njia pekee ni kuuza mazao yao ili walipe madeni na sio vinginevyo”

Lakini pia wapo wanaofanya kazi yao ni  kilimo kama sehemu ya kuendesha maisha yao hao wapo pamoja na wafanya biashara wanatakiwa kunufaika na bei hii ambayo kwa sasa itakuwa na tija kuliko kulanguliwa na wafanyabiashara”alisema akisisitiza

Iko haja ya Serikali kuongeza fedha za kutosha ili iweze kununua mazao haya ambapo hadi sasa kuna zaidi ya gunia elfu kumi zaidi ya lengo la Seriali huku wakulima wakiwa wametumia gharama kubwa kuleta bidhaa zao

Wakati huo wakulima hao wameitaka Serikali Wilayani Kiteto pamoja na uongozi wa juu kufika katika soko hilo kuona changamoto zinazowakabili na ambazo zinadaiwa kama hazitatatuliwa zinaweza kuzoroteza zoezi hilo

Mwisho

Maoni