KINNAPA latimiza ndoto za kamati za shule Kiteto



KINNAPA latimiza ndoto za kamati za shule Kiteto

Na. Mohamed Hamad MANYARA
SHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la KINNAPA wilayani Kiteto mkoani Manyara limetimiza ndoto ya baadhi ya kamati za shule za msingi kwenda ziara ya kimafunzo Kibaha mkoani Pwani ili ziweze kujua majukumu yao

Akieleza kazi zinazofanywa na shirika mbele ya wajumbe wa kamati za shule za msingi wilayani Kiteto na Kibaha ya Pwani mratibu wa kitengo cha elimu Shirika la KINNAPA Ngaringe Maitey alisema kuwa ni pamoja kuboresha usafi na mazingira kwenye shule na zahanati (wash project}

Kuhakikisha upatikanaji wa mali elimu bora na kujenga uwezo kwa wananchi (Kiteto livelihood support) Kuhakikisha ushiriki wa jamii katika miradi ya umma kufuatilia kusimamia kutathmini matumizi ya mali za umma (Public accounterbility)

Nyingine ni mwanzo bora (nutrition),(small holder group development) kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi kwa wakulima wadogo Kiteto,pamoja na kuboresha ulinzi wa nyanda za juu za lalisho ya mifugo



“Baadhi ya wajumbe wa kamati za shule za msingi hawajui mjukumu yao ipasavyo hali inayofanya elimu kudorora na kusababisha manung’uniko makubwa kwa wananchi juu ya Serikali yao iliyopo madarakani”

“Hatufanyi kazi za KINNAPA bali tunatekeleza majukumu ya Serikali, kila mtu ana wajibu wa kufanya kazi kwa ufanisi na katika hatua hiyo KINNAPA tunazijengea uwezo kamati za shule ili ziweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo”alisema Ngaringe

Kwa upande wake Melubo Ole Naiganya mwenyekiti shule ya msingi Irkiushibour alisema, awali hakuwa anafahamu majukumu ya kamati za shule hivyo kushindwa kutimiza wajibu wake na kusababisha shule kudhorota kielimu

Alisema elimu aliyoipata kutoka shirika la KINNAPA pamoja na ziara ya kimafunzo shule ya msingi Tumbi iliyopo Kibaha mkoani Pwani atahakikisha anatimiza wajibu wake kulinda shule yake kwa kusimamia miradi na kubuni…mingine

“Sikuwa najua kitu pamoja na kwamba wazazi waliona nafaa kwa kunichagua ili kushika wadhifa huo toka mwaka 2013 lakini baada ya kujegewa uwezo naamini kuwa nitawajibika ipasavyo katika nafasi hii ili nilete tija kwa shule yangu”alisema

Naye Mwenyekiti wa shule ya msingi Engusero engine Wilbrod Mathayo alisema ataiga mafanikio aliyoyaona shule ya msingi Tumbi ambayo yamesababishwa na umoja wa kamati hiyo ambayo imekuwa ya kuigwa

“Najua kuna kazi kubwa iliyofanyika hapa Tumbi na ndio maana tumeona mambo mengi mazuri hivyo naahidi katika shule yangu changamoto zilizopo nazibadilisha kuwa fursa ya kujiletea maendeleo kwa wananchi wangu”alisisitiza

Awali akieleza mafanikio ya shule hiyo Khamis Mbonde mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Tumbi alisema siri ya mafanikio ya shule yake ni pamoja na kuwepo kwa mipango imara inayoungwa mkono na wazazi katika utekelezaji

“Kabla ya kufanya jambo lolote hapa shuleni kwanza tunashirikisha wazazi ambao wao ndio wenye uchungu na shule hii hivyo wao ndio wenye maamuzi ya mwisho na wala hatuwalazimishi kwa jambo lolote” alisisitiza Mbonde

Mwalimu mkuu wa shule hiyo bw Jani Moses alisema pamoja na mafanikio yaliyofikiwa na shule yake bado anahitaji shirika la KINNAPA kuona namna ya kusaidia baadhi ya changamoto zinazowakabili katika shule yake kwakuwa ni shirika

Alisema shule yao inakabiliwa na uhaba wa madawati vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za waalimu hivyo wangependa kuona shirika la KINNAPA lililoweka ubia na wao lione namna ya kusaidia changamoto zilizopo

Mwisho
 



KINNAPA latimiza ndoto za kamati za shule Kiteto

Na. Mohamed Hamad MANYARA
SHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la KINNAPA wilayani Kiteto mkoani Manyara limetimiza ndoto ya baadhi ya kamati za shule za msingi kwenda ziara ya kimafunzo Kibaha mkoani Pwani ili ziweze kujua majukumu yao

Akieleza kazi zinazofanywa na shirika mbele ya wajumbe wa kamati za shule za msingi wilayani Kiteto na Kibaha ya Pwani mratibu wa kitengo cha elimu Shirika la KINNAPA Ngaringe Maitey alisema kuwa ni pamoja kuboresha usafi na mazingira kwenye shule na zahanati (wash project}

Kuhakikisha upatikanaji wa mali elimu bora na kujenga uwezo kwa wananchi (Kiteto livelihood support) Kuhakikisha ushiriki wa jamii katika miradi ya umma kufuatilia kusimamia kutathmini matumizi ya mali za umma (Public accounterbility)

Nyingine ni mwanzo bora (nutrition),(small holder group development) kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi kwa wakulima wadogo Kiteto,pamoja na kuboresha ulinzi wa nyanda za juu za lalisho ya mifugo



“Baadhi ya wajumbe wa kamati za shule za msingi hawajui mjukumu yao ipasavyo hali inayofanya elimu kudorora na kusababisha manung’uniko makubwa kwa wananchi juu ya Serikali yao iliyopo madarakani”

“Hatufanyi kazi za KINNAPA bali tunatekeleza majukumu ya Serikali, kila mtu ana wajibu wa kufanya kazi kwa ufanisi na katika hatua hiyo KINNAPA tunazijengea uwezo kamati za shule ili ziweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo”alisema Ngaringe

Kwa upande wake Melubo Ole Naiganya mwenyekiti shule ya msingi Irkiushibour alisema, awali hakuwa anafahamu majukumu ya kamati za shule hivyo kushindwa kutimiza wajibu wake na kusababisha shule kudhorota kielimu

Alisema elimu aliyoipata kutoka shirika la KINNAPA pamoja na ziara ya kimafunzo shule ya msingi Tumbi iliyopo Kibaha mkoani Pwani atahakikisha anatimiza wajibu wake kulinda shule yake kwa kusimamia miradi na kubuni…mingine

“Sikuwa najua kitu pamoja na kwamba wazazi waliona nafaa kwa kunichagua ili kushika wadhifa huo toka mwaka 2013 lakini baada ya kujegewa uwezo naamini kuwa nitawajibika ipasavyo katika nafasi hii ili nilete tija kwa shule yangu”alisema

Naye Mwenyekiti wa shule ya msingi Engusero engine Wilbrod Mathayo alisema ataiga mafanikio aliyoyaona shule ya msingi Tumbi ambayo yamesababishwa na umoja wa kamati hiyo ambayo imekuwa ya kuigwa

“Najua kuna kazi kubwa iliyofanyika hapa Tumbi na ndio maana tumeona mambo mengi mazuri hivyo naahidi katika shule yangu changamoto zilizopo nazibadilisha kuwa fursa ya kujiletea maendeleo kwa wananchi wangu”alisisitiza

Awali akieleza mafanikio ya shule hiyo Khamis Mbonde mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Tumbi alisema siri ya mafanikio ya shule yake ni pamoja na kuwepo kwa mipango imara inayoungwa mkono na wazazi katika utekelezaji

“Kabla ya kufanya jambo lolote hapa shuleni kwanza tunashirikisha wazazi ambao wao ndio wenye uchungu na shule hii hivyo wao ndio wenye maamuzi ya mwisho na wala hatuwalazimishi kwa jambo lolote” alisisitiza Mbonde

Mwalimu mkuu wa shule hiyo bw Jani Moses alisema pamoja na mafanikio yaliyofikiwa na shule yake bado anahitaji shirika la KINNAPA kuona namna ya kusaidia baadhi ya changamoto zinazowakabili katika shule yake kwakuwa ni shirika

Alisema shule yao inakabiliwa na uhaba wa madawati vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za waalimu hivyo wangependa kuona shirika la KINNAPA lililoweka ubia na wao lione namna ya kusaidia changamoto zilizopo

Mwisho


Maoni