KINNAPA
na mkakati wa kuboresha elimu Kiteto
Na. Mohamed Hamad Manyara
SHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la KINNAPA wilayani
kiteto mkoani Manyara katika kitengo chake cha elimu, limeanza kuzijengea uwezo
kamati za shule za msingi ili kujua majukumu yao
Jumla ya wajumbe 40 kutoka vijiji 20 vya
Partimbo,Kaloleni,Matui, Engusero engine,Ndirigish, njia panda,
Dosidosi,Ormaroroi,Ilkiushbaour,Lesoit,orgine, Emart,Makami,
Ngabolo,Njoro,Orpopong’I
Vijiji vingine ni pamoja Ilera,Mbigir, Lerug,Kijungu,
ambao kwa pamoja wanaendelea kujengewa uwezo na shirika hilo ili waweze kutenda
majumu yao wanapokuwa mahali pa kazi
Akieleza malengo ya mafunzo hayo mratibu wa kitengo hicho
bw. Ngaringa amesema uchunguzi
uliofanywa na shirika hilo
umebaini kuwa wajumbe wengi wa kamati za shule wilayani humo hawajui wajibu wao
Alisema kutojua wajubu wao kumechangia kushusha kiwango
cha elimu hasa pale wanaposhindwa kuhoji,kusimamia majukumu waliopewa na
wananchi shuleni
“Tumeona kuwa kuna haja ya kutoa elimu kwa kamati ili
waweze kujua wajibu wao wanapokuwa katika majukumu yao mara baada ya
kuchaguliwa na wananci katika nafasi hizo”
Amesema njia pekee ya kuinua kiwango cha elimu wilayani Kiteto
ni kuwajengea uwezo wadau wa elimu ili waweze kusimamia shule zao ipasavyo wakiwemo
waalimu wakuu waratibu wa shule pamoja na kamati zenyewe
Hata hivyo changamoto kubwa zimeelezwa kujitokeza katika
kuboresha elimu ya msingi ambazo zimechangiwa na ukosefu wa uwajibikajipamoja
na elimu duni kwa wajumbe ama viongozi waliopewa mamlaka
Wajumbe hao wamezitaka mamlaka zinazohusika na elimu ikiwemo
Serikali na mashirika ya umma kuendelea kuzijengea uwezo kamati za shule ili
ziweze kutenda majukumu yao ipasavyo
Mwisho
Maoni
Chapisha Maoni