SILAHA ZAMOTO ZAIDI YA 200 ZAKAMATWA KITETO





Zaidi ya Bunduki 200 zakamatwa Kiteto

Na. Mohamed Hamad Kiteto
Matukio ya kihalifu yanayoendelea kujitokeza wilayani Kiteto mkoani Manyara yamelazimu Jeshi la Polisi wilayani humo kukusanya silaha aina ya bunduki zinazomilikiwa kihalali na isivyo halali ili kubaini zilizotumika kufanya uhalifu

Zaidi ya bunduki 200 za aina tofauti zikiwemo Raifo,Shotigan,na Magobole zimekusanywa wilayani humo kwa lengo la kufanya uchunguzi kama zimehusika katika mauaji ya watu saba yaliyotokea hivi karibuni katika vijiji vya Chekanao na Matui

Awali akizungumza na vyombo vya habari Deosdedit Nsimeck Kamanda wa Polosi wa Mkoa wa Manyara mjini Kibaya alisema hatua hiyo inasaidia kubaini silaha zinazofanya  matukio ya kihalifu  katika maeneo mbalimbali Wilayani humo

“Silaha hizo toka kwa wananchi tumeamua kuzikusanya zikiwemo zile zinazomilikiwa kihalali na isivyo halali ili kudhibiti vitendo vya kihalifu vinavyoendelea kujitokeza vikiwemo vya mauaji ya mara kwa mara”alisema Nsimeck

Wananchi na viongozi katika maeneo tofauti wamepongeza kitendo hicho wakisema hatua hiyo ni busara iliyotumika ambayo itakomesha mauaji pamoja na kuwepo kwa changamoto kubwa katika kuzipata huko vijijini

“Wakati mwagine mmiliki wa Silaha husika kihalali analazimika kuingia mitini akiwa hana nia ya kuikabidhi lakini baadaye anaagizia mke wake kwenda kuikabidhi kutokana na sababu zao mbalimbali” alisema mmoja wa maafisa hao

Kwa upande wake Emanuel Papian mjumbe wa NEC (CCM) Taifa akizungumzia hatua hiyo alisema matukio hayo yatapungua  kutokana na jitihada hizo na kulitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha watuhumiwa wanafikishwa mahakamani

“Utakuta mhalifu anafanya atakavyo mf. mauaji yanayo endelea kutokea Kiteto hutasikia aliyefanya matukio anawajibishwa, na hili linaenda sambamba na kutowajibika kwa viongozi wa ngazo mbalimbali za maamuzi”alisisitiza MNEC huyo

Katika hatua hiyo mjumbe huyo aliwataka wananchi Wilayani Kiteto kujipima kama wanatosha katika nafasi wanazoshikilia ili kuepusha manunguniko kwa wananchi ambayo yanajitokeza kila mara

Natamani siku moja nisikie na kuona wananchi wa Kiteto wanaishi kwa amani na kujivunia viongozi wao waliowachagua kuwa wanasikilizana katika shuhuli zao mbalimbali za kujiletea maendeleo

Mwisho

Maoni