KITETO YATAKIWA KUJENGWA UPYA


Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Emmanuel Papian akiwa katika picha ya pamoja na na jamii ya kifugaji wamasai hivi karibuni kata ya matui wilayani Kiteto

Kiteto yatakiwa kujengwa upya

Na. Mohamed Hamad Manyara
MJUMBE wa halmashauri kuu ya CCM Taifa Emmanuel Papian amevunja ukimya na kusema wilaya ya Kiteto inatakiwa kujengwa upya kwa misingi ya watu kupendana, kuondoa chuki,ubaguzi wa kikabila,rushwa na ubinafsi

Akizungumza hayo mjini kibaya MNEC huyo hivi karibuni alisema wakulima na wafugaji wanachuki dhidi ya baadhi ya viongozi wa Serikali kutokana na kutotatuliwa matatizo yao kwa muda mrefu

“Huwezi kuamini hatua iliyofikiwa na wananchi wa kiteto ni kuuana kwa kuchinjana,kupigana risasi,kukatana mapanga hadi kufa na hii ni kutokana na kukosekana kwa usimamizi mzuri wa ardhi”

Alisema pamoja na kuwepo kwa sheria ya ardhi ambayo inatakiwa kusimamiwa na viongozi waliopo madarakani tatizo lililopo ni kukosekana kwa uadilifu dhidi ya baadhi ya viongozi wa Serikali hivyo kuwagombanisha wananchi  hao

“Utamkuta kiongozi anawezo wa kuongea na kundi moja tu la baadhi ya wananchi wake huku wengine wakitengwa hali hii inachangia sana mgogoro huu na ilipigwa vikali na Baba wa Taifa letu mwalimu Nyerere”alisema Papian

Akitoa suluhisho la mgogoro huo wa Kiteto alisema njia pekee ya kukabilia tatizo hili ni viongozi kuacha tabia za kuongoza kwa misingi ya ubaguzi hasa kwa wengine kuitwa wazawa na wengine wahamiaji

Nchi ya Tanzania imejengwa kwa misingi ya umoja udugu na mshikamano kazi ambayo ilifanywa vizuri sana na mwasisi wetu baba wa taifa lakini leo utasikia Kiongozi anasimama jukuwaani akiwaita watanzania wenzake kuwa ni wavamizi,

“Mtu hawezi kuwa mvamizi ndani ya nchi yako kwani kila mtu ana haki ya kuishi mahali popote ilimradi asivunje sheria, sasa hili limegawa wananchi na kujiona kuwa wanahaki ya kuchukua hata sheria mikononi kama kuua wenzao”

Alisema unaweza kuona mtu anaamua kumchinja mwenzake kasha mwisho wa siku unasikia waliouawa ni watu wa kuja sio wenyeji Serikali inaliona naiomba sheria ifuate mkondo wake na tuwe wazalendo”alisisitiza

Naamini kuna kazi kubwa inayofaywa na Serikali ikiwemo kubaini mipaka,kutenga maeneo ya matumizi bora ya ardhi pamoja na kuongeza vituo vya polisi “wananchi tumieni nafasi hiyo kuhakikisha tunaijenga Kiteto upya na viongozi tuongee na makundi yote ndani ya jamii na sio kuwatenga”alisema Papiani

Mwisho

Maoni