TUME:KITETO WEKENI MABANGO KWENYE MAENEO TENGEFU

 Makamu mwenyekiti wa Halmasauri ya wilaya ya Kiteto Lairumbe Mollel akifafanua jambo kwenye kikao cha baraza la madiwani pembeni yake ni Bosco Ndunguru DED Kiteto Manyara Picha na Mohamed Hamad

Tume: Kiteto wekeni mabango kwenye hifadhi

Na. Mohamed Hamad Manyara
Tume maalumu toka ofisi ya Waziri Mkuu iliyowasili Kiteto mkoani manyara kushughulikia migogoro ya ardhi imeutaka uongozi wa wilaya kuweka mabango kwenye maeneo yaliyopangwa matumizi bora ya ardhi

Hayo yameelezwa na kiongozi wa tume hiyo hakutaka jina kutajwa akizungumza na Jambo leo kuhusu hatua iliyofikiwa na tume iliyodaiwa kuwa itafanya kazi kwa  miezi miwili na nusu  kuhakikisha migogoro imamalizika

“Kazi ya kuhakiki mipaka ya Hifadhi ya Emboley Murtangos kwa hatua ya kwanza na ya pili imekamilika,tunataka Halmashauri iweke mabango kuonyesha hifadhi hiyo kuepuka watu kuingia na kufanya kazi za kibinadamu” alisema Kiongozi huyo

Pia alisema katika kuhakikisha kazi hiyo inafanikiwa kwa kiwango kizuri zaidi aliitaka Halamshauri ya Wilaya kutengeneza mkuza (barffer zone) utakaosaidia kutenganisha eneo hiyo na maeneo mengine ambayo yamepakana

Hata hivyo kucheleweshwa kuwekwa mabango hayo kunahofiwa kuwa watu wataweza kuingia kinyemela kwenye maeneo hayo yaliyotengwa na kufanya shuhuli za kibinadamu kazi ambayo imepigwa marufuku

“Kwa sasa hatakiwe kuwepo mkulima wala mfugaji kwenye Hifadhi ya Emboley Murtangos Serikali imeamua kurejesha eneo hilo katika uoto wake wa asili kwa kutoona shughuli zozote za kibinadamu humo”alisema kiongozi huyo

Awali baadhi ya Viongozi wilayani Kiteto walieleza wananchi kuwa eneo hilo ni kwaajili ya hifadhi ambayo wafugaji wanaweza kuingiza mifugo yao humo na kutoka jambo ambalo lilizu mgogoro hivyo wakulima nao wakaamua kuingia kwa nguvu na kuanza kulima

“Tumeweka taratibu zote za kitaalamu humo eneo sasa linafahamika na kutambulika kilichobakia ni kusimamia sheria ipasavyo na hapo ndiko kwenye matatizo kwa baadhi ya viongozi mbalimbali hapa nchini kushindwa kuwajibika”alisisitiza

Serikali imetumia fedha nyingi kutuma wataalamu 27 wa fani mbalimbali kufanya kazi kwa zaidi ya miezi miwili kama kutakosekana  dhamira safi kusimamia kazi hii matatizo haya yataendelea kujirudia alisisitiza kiongozi huyo

Baadhi ya wananchi wilayani hapo waliitaka Serikali kuhakikisha kazi hiyo inakamilika mapema sambamba na kuwekwa alama za mabango makubwa ili yabainike wasiweze kuingia ndani ya maeneo ambayo hayaruhusiwi na yanaweza kuleta migogoro

Mwisho

Maoni