MADAWA YA 94 MIL KITETO KUTEKETEZWA


 Kaimu mganga mkuu  wa Hospitali ya Wilaya ya Kiteto Dr Kongora akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake kuhusu madawa ya 94 mil kutakiwa kuteketezwa Picha na Mohamed Hamad Manyara


Madawa ya 94 mil kuteketezwa Kiteto

Na.Mohamed Hamad Manyara
Imeelezwa kuwa aina mbalimbali za madawa baridi ya binadamu ya thamani ya 94 mil katika Hospitali ya wilaya ya Kiteto mkoani Manyara yanakusudiwa kuteketezwa baada ya kubainika kuwa yamekwisha muda wake (expired date)

Hayo yameelezwa na Kaimu mganga mkuu wa Hospitali ya wilaya ya Kiteto Dr. Marting Kongora akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake waliotaka kujua changamoto zinazoikabili sekta ya Afya wilayani humo

“Tuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa aina ya dawa ambazo zinachangiwa na bohari kuu MSD kuwa hawaleti dawa kwa wakati na wanapoleta wakati mwingine wanayaleta yakiwa muda wake umebaki mchache”

Alisema kuwa madawa mbalimbali ya thamani ya 94 mil ya kuanzia mwaka 1990 yakiwemo ya kurefusha maisha ARVs,TB na ya Maleria yanatakiwa kuteketezwa baada ya kwisha muda wake

“Tunachofanya hapa Hospitali ni kupitia katika Zahanati zote na vituo vya Afya kukagua madawa na tunapobaini kuwepo tunayakusanya na kuyahifadhi mpaka tupate kibali ama ruhusa ya kuyateketeza”alisema Dr.Kongora

Hata hivyo changamoto ya kuteketeza madawa hayo imejitokeza baada ya kukosemana fedha za uteketezaji pamoja na kutoandaliwa eneo maalumu kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi

Kwa upande wa wananchi waliozungumzia kuhusu zoezi hilo walishangazwa kusikia kuteketezwa kwa madawa hayo wakidai wakati wote waliambia kunaupungufu wa dawa Hospitalini

“Inakuwaje dawa hizo zinateketezwa wakati kila ukifika Hospitali ama Zahanati unaambiwa nenda kanunue dawa maduka ya watu binafsi hizi zilizoharibika zilikuwa wapi na kwanini hazikutolewa wakati wa kuhitajika?alihoji Joseph Kaaya (mwananchi)

Mwisho

Maoni