WASAIDIDI WA KISHERIA 25 WAJENGEWA UWEZO NA CELG


 CELG na mkakati wa kuwajengea uwezo wasaidizi wa kisheria Kiteto Picha na Mohamed Hamad Manyara


Wasaidizi 25 wa kisheria  kiteto wajengewa uwezo

Na Mohamed Hamad Manyara
Jumla ya wasaidizi wa kisheria 25 kutoka katika kata mbalimbali wilayani Kiteto Mkoani Manyara wameanza kupatiwa mafunzo ya siku tano kwa lengo la kuwajengea uwezo katika kazi zao

Awali akifungua mafunzo hayo Joseph Mwanga akimwakilisha Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto alisema mafunzo hayo ni mwafaka wakati huu kutokana na kuwepo changamoto za za ukatili wa kijinsia na migogoro ya ardhi

“Kiteto inatambulika sana hapa nchini kwa migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na kwamba mafunzo haya yatakuwa mwarubaini wa tatizo hilo”alisema Mwanga

Kwa upande wake mwezeshaji Mjengi Lissu wakili wa Kituo cha sheria za mazingira na utawala bora (CELG) ambacho makao yake makuu yapo Mbezi Beach Dar es  Salaam alisema baada ya washiriki kumaliza mafunzo hayo watafanya kazi kwa kipindi cha miaka miwili wilayani humo

Alisema CELG inafanya kazi katika mikoa yote ya Tanzania bara katika Nyanja za elimu kwa jamii kuhusu sheria mbalimbali za mazingira,maliasili na haki za binadamu

Pia kutoa msaada wa kisheria kwa jamii pamoja na usuluhishi wa migogoro inayohusu masuala ya mazingira,ardhi na maliasili

Hata hivyo alisema kuwa Kituo kinaendelea kutoa msaada wa kisheria kwa jamii katika wilaya ya Mafia Rufiji na Bwagamoyo chini ya ufadhili wa Legal Service Facility

Pia kinatoa elimu ya kisheria ya utatuzi wa migogoro  ya ardhi na matumizi endelevu ya ardhi katika wilaya ya Rufiji chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society

Kuwezesha jamii juu ya utunzaji wa rasilimali za misitu na ufugaji bora wa nyuki katika misitu ya Zumbi,Kikale,na Ngumburuni wilaya ya Rufiji chini ya ufadhili wa mfuko wa Taifa wa Msitu   (TFF)

Ambapo sasa kituo kinatekeleza na mradi wa kulinda wanawake dhidi ya ukatili wa kijinsia katika wilaya ya Hanang na kiteto mkoani Manyara chini ya ufadhili wa LSF  kwa muda wa miezi 30 kwa lengo la kupunguza ukatili dhidi ya wanawake

Alisema kuwa pamoja na mambo mengine Kituo kinalenga kuwa ifikapo 2016 huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia,kuongeza uwajibikaji katika jamii na kuwezesha wanawake kulinda na kutetea haki zao kitafanikiwa

Kwa upande wa Mashaka Fundi,Mwadawa Ally,Musa Chambali na Janne Isangya washiriki katika mafunzo hayo walisema ukatili wa kijinsia wilayani Kiteto umekithiri na kwamba mafunzo hayo ni mwafaka kwa sasa

Walisema kesi nyingi zimeongezeka mahakamani katika ubakaji,kulawiti,ambapo wamedai pamoja na jitihada hizo jamii imetakiwa kuwa tayari kupokea elimu kutoka kwa wasaidizi hao

Mwisho

Maoni