Wakulima 9 Kiteto wanusurika kuuawa,walazwa


Wakulima 9 Kiteto wanusurika kuuawa,walazwa
·        Kamati ya Pinda yaenda kuwapa pole

Na. Mohamed hamad Kiteto
Jumla ya wakulima 9 wa kijiji cha Kimana kata ya Partimbo wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto baada ya kukatwakatwa mapanga pamoja na kuchomwa mikuki wakiwa shambani na jamii ya kifugaji wamasai

Tukio hilo limetokea march 31 mwaka huu katika maeneo tofauti ya kata ya Partimbo ambako jamii ya kifugaji wamasai wamedaiwa kuendeleza ukaidi wa agizo la Serikali la kujichukulia  sheria mkononi kuvamia wakulima shmbani na kuwapiga

Waliojeruhiwa ni pamoja na Hamidu majidi (42) wa eneo la katikati Jaki Mgomba (32) wa eneo la Kisima, Sefu Frenki (33) wa eneo la kisima, na mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Ramadhani ambaye alijeruhiwa sehemu za kichwani

Wengine ni Kizota Saitoti (35),Paulo Disulile (39) wa kisima aliyevunjwa mkono, Yahaya Mussa (33) aliyejeruhiwa kichwani na kuvunjwa kidole cha mkono,Mbaya Malogo (42) na mmoja ambaye alijulikana kwa jina moja la Yusuph

“Tunachoshangaa toka tumepata matatizo haya hakuna kiongozi yoyote wa Serikali ya Kiteto aliyefika japo kutupa japo pole kwa tunayofanyiwa na hawa wenzetu wamasai hatujui wanafurahishwa ama vipi”alisema Jaki Mgonda majeruhi aliyechomwa mkuki kiunoni

Alisema kutofika kwa viongozi hao wa wilaya ni picha tosha kwa umma kuwa kuna jambo lililojificha akidai kama kuna mahali pa kuanzia kufuatilia kujua ukweli wa sakata hili ni kuanzia hapo kwani hakuna sababu zozote za msingi wao kutofika wakati ofisi zao ziko karibu na Hospitali ya wilaya na ndipo wanapopita kwenda mahofisini

Alienda mbali zaidi akisema kama tume iliyoundwa na Waziri Mkuu kwaajili ya kutafuta ufumbuzi wa migogoro hiyo walifika hospitalini na kutoa pole wao walipata uchungu gani na kwanini viongozi wa eneo husika  huwa hawafiki alihoji

Viongozi wa wilaya waliotarajiwa kufika ni pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Kimiang’ombe  Nzoka na wengine ambapo baada ya kutafutwa kwa njia ya simu juu ya lalamiko hilo hawakupatikana

“Inaumiza sana kuona viongozi wetu wa wilaya wanaonekama kuwa mstariu wa mbele kubagua watu kwa kutoshirikiana nasi  mpaka tume ya Waziri Mkuu iguswa na kufika ili hali siku zote wapo na wanaonekana mitaani na magari yao alisema ambapo alidai walichomwa mikuki,

Kukatwakatwa mapanga pamoja na kushambuliwa kwa fimbo sehemu mbalimbali za miili yao”alisema kwa uchungu mhanga Jaki aliyekuwa na jeraha la mkuki kiunoni akidai ubaguzi ni mkubwa

Kwa mujibu wa taarifa za uhakika kutoka ndani ya kamati ya Pinda iliyopo Kiteto zilisema baada ya kusikia tukio hilo mara moja walifika na kushuhudia majeruhi hao ambao wengi wao walikuwa na mjeraha mbalimbali ya miili yao wakiwemo wale waliochomwa mikuki na mwingine kuvunjwa mkono

“Tulifanya mahojiano na wahanga kwakweli vitendo hivi ni vibaya sana kuna haja gani wewe mfugaji kuingiza mifugo yako shambani kwa nguvu halafu unampiga mkulima haya mamlaka umepata wapi wakati nchi hii inaongozwa kwa sheria”alisema mmoja wa wanakamati hiyo

Mwisho






Maoni