22 wafanyiwa Oparesheni ya macho Kiteto




22 wafanyiwa Oparesheni ya macho Kiteto

NA MOHAMED HAMAD MANYARA
JUMLA ya watu 22 wenye matatizo la macho wilayani Kiteto mkoani Manyara, wamefanyiwa operesheni za kuondoa mtoto wa jicho pamoja na mtindio wa maji kwenye macho

Operesheni hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika kituo cha macho  cha kanisa la Anglikan Dayosisi  ya Kiteto ADC kwa ushirikiano na madaktari kutoka hospitali ya Mvumi iliytopo mkoani Dodoma

“Watu hawa hawakuwa wanauwezo wa kuona, walishikwa mkono kipindi chote na hata walipofika hapa kituoni lakini baada ya kufanyiwa operesheni wanaoona naamini wanafuraha kubwa”alisema Sis Sarawek Mbwelwa mratibu wa macho Kiteto

Alisema Kituo cha ADK Kiteto kimekuwa na utaratibu wa mara kwa mara kuwafanyia operesheni watu wenye matatizo ya macho kuwaondolea upofu hali iliyowafanya wakate tamaa ya kuishi maisha ya duniani

Kwa upande wake Elizabeth Masai mmoja wa wanajamii ya kimasai wilayani humo alisema baada ya kupata matatizo ya macho aliishi kwa kushikwa mkono na kufanyiwa kila kitu lakini baada ya kufanyiwa operesheni sasa anaona

Alisema Kitengo cha macho cha ADK kimekuwa msaada mkubwa sana kwake kwani hakuwa ananufaika na mamisha ya ulimwenguni na alikata tamaa ya kuendelea kuishi akisema alitamani kuwa bora amekufa kwa adha alizopata akiwa haoni


Akizungumzia matatizo ya macho wilayani humo Sis Mbwelwa alisema adha hiyo inaongezeka siku hadi siku  wilayani humo kutokana mazingira ya maisha ya wananchi yakiwemo ya uhaba wa maji na kuwa na vumbi kipindi kirefu kwa mwaka

Katika kukabiliana na matatizo  hayo ya macho alitoa wito kwa wananchi kuwa na utamaduni wa kupima macho mara kwa mara kisha kuchukua hatua ya tiba ambayo ndio mwarubaini wa matatizo hayo

Baadhi  ya wananchi wamepongea jitihada za ADK kuwaondolea adha ya upofu wahanga hao wa macho wakisema awali walitumia gharama kubwa kusaka huduma hiyo mbali ambako ni Dodoma na KCMC lakini  sasa inapatikana wilayani hapo

Mwisho

Maoni