Mabomu,risasi za moto zatumika ofisi za CCM Kiteto







Mabomu,risasi za moto zatumika ofisi za CCM Kiteto
·               
                   Gari la Ole Sendeka lavunjwa vioo,Ole Nangoro anusurika kichapo
·                Nyumba yake yavamiwa na wanachama, wavunja taa na kumpiga mlinzi

Na. Mohamed Hamad Manyara
JESHI la polisi wilayani Kiteto mkoani Manyara limetumia mabomu ya machozi na silaha za moto kuokoa aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro na Christopher Ole Sendeka pamoja na kamati ya siasa ya Mkoa wa Manyara waliofika kuhakiki matokeo ya Ubunge

Awali wajumbe hao walizuiwa kwa mawe na magogo barabarani kata ya Engusero wasifike makao makuu ya wilaya ya Kiteto wakitokea Dodoma, hali iliyolazimu Jeshi la Polisi kuwaokoa kwa kuwapa ulinzi kwa kuwafikisha Kibaya kwaajili ya kuhakiki matokeo hayo

Baada ya kamati ya siasa ya mkoa kufika katika ofisi za CCM Wilaya ya Kiteto majira ya mchana walianza kuhakiki matokeo ya Ubunge ambayo yalidaiwa kulalamikiwa na aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro aliyeambatana na wajumbe hao kutaka yahakikiwe

“Baada ya kusikia kuna kamati ya siasa mkoa wa Manyara imefika wanachama tulilazimika kufika ofisi za CCM kutaka kujua hatma ya ujio wao, kwani tumeshuhudia maeneo mengi matokeo ya uchaguzi yanabadilishwa baada ya kutangazwa washindi”alisema mwananchi Rajabu Jagon

Alisema wajumbe hao waliingia ofisini ya CCM kwa zaidi ya masa 6 huku wanachama wakisubirinje hali iliyohofiwa kuwa huenda walilenga kubadilisha matokeo hayo na ndipo kauli za kejeli vitisho zikaanza kutolewa na baadhi ya wajumbe hao na kuwafanya wanachama wapandwe na jazba

Christopher  Ole Sendeka mjumbe wa kamati ya Siasa mkoa wa Manyara  baada ya kutoka nje alionekana kuibua malumbano na wanachama hao wakidai aliwakashifu hali iliyowapandisha jazba vijana hao na kuanza kurusha mawe kutaka kumpiga hali iliyowafanya polisi kuingilia kati kunusuru

Muda mfupi Christopher Ngubiagoi mjumbe wa Halamshauri kuu ya CCM Taifa aliyefuatana na kamati hiyo alitoka nje kutuliza mzuka wa wanachama hao bila mafanikio na ndipo mawe yalipoanza kurushwa na kuvunjwa kioo cha nyuma cha gari la Ole Sendeka na ndipo Polisi wakaanza kurusha mabomu na silaha za moto juu

Tukio hilo lilichukua takriban dakika arobaini na tano baada ya wanachama hao kupambana ana kwa ana na polisi ofisini hapo huku wakijaribu kuwaokoa wajumbe kwa kuwalazimisha watoke kwenye ofisi hizo kwa kurusha mabomu na kutumia silaha za moto

Hii ni mara ya pili kwa mbunge anayemaliza muda wake Ole Sendeka kupata wakati mgumu baada ya dereba wake kumwondosha katika ofisi hizo mithili ya kukwepa majambazi huku akiendelea kushambuliwa kwa mawe hadi alipotoweka katika viwanja hivyo

Katika sakata hilo Jambo leo limeshuhudia uharibifu uliofanywa na wanachama hao kwenye nyumba ya aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kiteto Ole Nangoro ikiwa imevunjwa taa za nje kwa kama ishara ya kutomkubali katika utawala wake

Kwa mujibu wa Christopher Ngubiagaji mjumbe wa Halamshauri kuu ya CCM Taifa aliwaambia wanachama hao kuwa hawakuja kubatulisha matokeo, alitumwa na Katibu wa CCM Taifa Abdurahmani  Kinana kuhakiki matokeo hayo yaliyolalamikia na mmoja wa wagombea

Pia alisemba mbali na hilo alikuja kuona hali ya kisiasa kwa  mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM kama anaweza  kupambana na mgombea kupitia umoja wa vyama UKAWA ili kuwezesha CCM kuendelea kutawala

Kufuatia kauli hiyo mjumbe huyo alisema “mwenye macho haambiwi tazama,hana shaka na kilichoamuliwa na wana-CCM Kiteto na kwamba ataenda kumwambia Kinana kuwa maamuzi wa wanakiteto yanaeleweka ili naye aweze kufanya maamuzi yake

Kauli hiyo iliungwa mkono na katibu wa CCM Wilaya Abeid Maila aliyesema kilichotokea Kiteto hakihusishwi na kiongozi yoyote, bali wananchi waliamua kutaka kujua hatma yao kuwa walichokifanya ni sahihi na wala hawataki kibadiliswe

Mwisho

Maoni