Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WAZIRI MATATANI KWA KUNUNUA KALAMU @100$ , SAWA NA Tsh. 210,000 /= kwa kila kalamu




Waziri mmoja nchini Kenya amejipata taabani baada ya uchunguzi kugundua kuwa wizara yake ilinunua kalamu moja kwa dola 100.

Waziri wa ugatuzi bi Ann Waiguru, anatakiwa kufika mbele ya kamati ya bunge kuelezea ilikuwa vipi akatumia kiwango hicho cha fesha za umma.
Mbali na kalamu iliyogharimu dola 100, bi Waiguru pia alinunua runinga ya afisi yake kwa gharama ya dola $19,000,
Kipakatilishi (Laptop) kwa gharama ya dola $11,000 zulia ya afisi yake kwa gharama ya dola $ 3,800 programu ya kulinda kompyuta isiambukizwe virusi kapersky kwa gharama ya dola 9,737.
Programu ya Adobe kwa gharama ya $19,000.
Kifaa cha kutoa kondomu kiligharimu wiazara hiyo ya Ugatuzi dola $250 kila moja.
Waziri huyo sasa amesema kuwa hizo zote ni njama za kumpaka tope kwani yeye mwenyewe hana doa na kuwa ataendelea kuhudumia taifa kwa mujibu wa wajibu aliopewa na rais Kenyatta.

Chanzo jamiiForums

Maoni