MARAIS WALIOUWAWA KWA KUPIGWA RISASI


 
BAADA ya wiki iliyopita kuwaletea marais wa Afrika waliofia madarakani. Yaani walikuwa wakiongoza nchi zao wakakumbwa na mauti. Wiki hii tunawaletea marais waliouawa kwa kupigwa risasi wakiwa madarakani.

Abraham Lincoln.
ABRAHAM Lincoln; alikuwa Rais wa 16 wa Marekani. Aliuawa mwaka 1865 jijini Washington kwa kupigwa risasi kichwani kwa nyuma na John Wilkes. Alikuwa amekaa na mkewe. Bastola iliyotumika inaitwa Deringer.


Muhammar Muhamad Abu Migar al Ghaddaf.
MUHAMMAR Muhamad Abu Migar al Ghaddaf; alikuwa Rais wa Libya kwa miaka 42. Aliuawa kwa kupigwa risasi ya kichwa kwenye vurugu za kisiasa mjini Sirte, Libya, Oktoba 20, 2011.


John Francis Kennedy ‘JFK’.
JOHN Francis Kennedy ‘JFK’; ni Rais wa 35 wa Marekani. Aliuawa mwaka 1963 mjini Dallas kwa kupigwa risasi na Lee Harvey akiwa kwenye gari la wazi barabarani.


Indira Priyadarshini Gandhi
INDIRA Priyadarshini Gandhi; alikuwa Rais wa India. Aliuawa mwaka1984 kwa kupigwa risasi na walinzi wake, Satwant Singh na Beant Singh jijini New Delh, India.


Laurent Desire Kabila
LAURENT Desire Kabila; alimng’oa madarakani Rais Mabotu Seseko wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, lakini mwaka 2001 akauawa kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa ni walinzi wake.


Thomas Isdor Noel Sankara

THOMAS Isdor Noel Sankara; alikuwa Rais wa Burkina Faso Alitawala nchi kwa miaka 4 hadi 1984 alipouawa kwa kupigwa risasi na Blaise Compaore ambaye hivi karibuni ameikimbia nchi hiyo.
WILLIAM Richard Tolbert Jr; alipigwa risasi mwaka 1980 katika mapinduzi ya kijeshi akiwa Rais wa Liberia. Samuel Doe akiwa na cheo cha sajenti ndiye aliyetajwa kumuua.

 
Abeid Amani Karume
ABEID Amani Karume; alikuwa Rais wa Zanzibar tangu mapinduzi ya mwaka 1964. Aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa anacheza bao mwaka 1972 na mtu ambaye hakuwahi kupatikana.
 
 
NA
Jean baptist ouedraogo; aliitawala Burkina Faso kwa mwaka mmoja tu, 1982-83. Aliuawa kwa kupigwa risasi na Thomas Sankara ambaye alichukua madaraka ya kuiongoza nchi hiyo kabla na yeye kupinduliwa.

Maoni