Serikali Kiteto yabeba zigo la kutengeneza madawati




 Mkuu wa wilaya ya Kiteto Kanali Samuel Nzoka akichangia jambo kwenye kikao cha wadau wa elimu Kiteto Picha na Mohamed Hamad


 Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Kiteto Bosco Ndunguru akichangia jambo kikao cha wadau wa elimu jana

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Lairumbe Mollel akichangia jambo kwenye kikao cha wadau wa elimu Kiteto

 Afisa elimu Sekondari Rajabu Chongoe akitoa taarifa ya hali ya elimu Kiteto



 Afisa mkurugenzi wa udhibiti wa ubora wa shule Fidelis Kyarwenda akifafanua jambo

 Kaimu Afisa elimu shule za msingi Omar Mlekwa akitoa taarifa ya hali ya elimu Kiteto kwa wadau

 Mdau wa elimu kutoka hifadhi ya WMA Kiteto akichangia jambo

 DED na DAS Kiteto wakisikiliza jambo kwa makini kikao cha wadau wa elimu

wenyekiti wa SULEDO Sharifu Lemanda kwenye kikao cha wadau wa elimu Kiteto

 Uongozi wa wilaya ya Kiteto kushoto DED Bosco Ndunguru, anayefuata DAS Necodemus John, anayefuata DC Kanal Samuel Nzoka anayefuata Makamu mwenyekiti wa Halmashauri Yahaya masumbuko Picha na Mohamed Hamad Kiteto

Wanafunzi wa sekondari ya kibaya wilayani Kiteto hapo juu wakiwa kwenye jengo la maabara ambalo halijakamilika baada ya kukosa darasa huku wakiwa wamekaa chini kwa kukosa madawati picha na Mohamed Hamad


 Wadau wa elimu wilayani Kiteto wakiwa katika kikao kujadili changamoto zinazokabili sekta ya elimu wilayani humo Picha na Mohamed Hamad

 Shule ya Sekondari Kibaya hapo chini iliyoanzishwa miaka minne iliyopita inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa,nyumba za walimu,viti na meza, hali inayosababisha adha kwa wanafunzi katika masomo Picha na Mohamed Hamad


 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Kibaya wilayani Kiteto wakionyesha tofali wanazotumia kukalia baada ya kukosa viti na meza pamoja na darasa Picha na Mohamed Hamad Kiteto


NA.MOHAMED HAMAD
Serikali wilayani Kiteto mkoani Manyara imesema itahakikisha inamaliza tatizo la wanafunzi kukaa chini kwa kutengeneza madawati yanayotokana na  msitu wa mbao wa SULEDO uliopo wilayani humo

Akizungumza mbele ya kikao cha wadau wa elimu kilichofanyika march 10 mwaka huu, mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Bosco Ndunguru alisema alisema, Serikali imelazimika kutumia msitu wa SULEDO  kukabiliana na tatizo hilo

“Wakati mwingine watu wanaweza kukushangaa kiongozi wa eneo husika  juu ya tatizo la wanafunzi kukaa chini wakati tuna misitu kama ule wa SULEDO ambao unanufaisha maeneo mengine kwa suala la mbao”alisema Mkurugenzi huyo

Wakichangia uboreshaji wa sekta ya elimu Hassani Konki,Ramadhani Machaku,Ibrahimu Msindo wadau wa elimu wilayani humo walisema ili kuimarisha sekta hiyo viongozi wa Serikali hawana budi kutimiza wajibu wao

“Kiongozi wa Serikali tumempa mamlaka kusiomamia sheria zilizopo ikiwemo ya elimu, sasa kama wanashindwa na kubaki kulalamika kwa kutoa kisingizio cha wananchi hawana uelewa mzuri juu ya suala la elimu watatuchelewesha”

“Tunataka kusikia Serikali wilayani Kiteto ikitoa matamko mazito na hata kuchukua hatua dhidi ya watu wanaovunja sheria ili mwisho wa siku tuone elimu ikiimarika kwa wanafunzi kupata elimu”alisema Ibrahimu Msindo

Kwa upande wake Hassani Konki mdau wa elimu alisema, ili sekta ya elimu iweze kuimarika waalimu wanapaswa kupatiwa haki zao pamoja na kupunguza uhaba wa waalimu shuleni kwa kuajiriwa wengine akisisitiza haki huendana na wajibu

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Kanal Samuel Nzoka aliwataka wadau wa elimu kuona kuwa kuna wajibu wa kuchangia sekta hiyo kwa hali na mali kuwa elimu bure iliyosemwa na serikali haina maana ya mzazi hawezi kuchangia

Kwa upande wake kaimu afisa elimu shule za msingi Omari Mlekwa alisema wilaya inaupungufu wa madawati 7,777 kati ya 7,160 yaliyopo kutokana na uchangiaji hafifu wa wazazi kabla ya elimu bure

Afisa elimu sekondari Rajabu Chongowe akiwasilisha taarifa ya elimu kwa wadau hao alisema jumla ya viti 1478 na meza 1710 zinahitajika kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2016 ili waweze kusoma wakiwa wamekaa tofauti na ilivyo sasa wengi wao kukaa chini

‘Mhesimiwa mwenyekiti mkakati uliopo ni kwamba, tumeweza kuzungumza na uongozi wa hifadhi ya msitu wa SULEDO na kukubaliana nao kuwa watatengeneza madawati kwa bei ya kutusaidia ili kuondoa adha kwa wanafunzi hawa

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Lairumbe Mollel aliwashukuru wadau hao wakiwemo uongozi wa msiti wa SULEDO kwa kukubali kutengeneza madawati kwa bei ya chini, pamoja na uongozi wa umoja wa vijiji vilivyounga hifadhi ya wanyama WMA kwa kusaidia sekta ya elimu madawati pamoja na vyumba vya madarasa

Mwisho

Maoni