DC Sara awaonya wanovamia Mashamba.

john walter


MKUU wa wilaya ya Hanan’g  Sara Msafiri amewatangazia kiama wananchi wanaodaiwa kuwa  wavamizi wa shamba la mwekezaji katika  kijiji cha  Min’genyi   kata ya Gehandu na kuwapa  masaa 24 kuwa wametoweka  ndani ya shamba  hilo.



Kiama hicho aliwatangazia wavamizi hao jana wakati  akiwahutubia  wananchi wa kijiji hicho waliofurika kumsikiliza mkuu huyo wa wilaya ili kufahamu atawafanyaje wavamizi hao wanaotamba kuishinda serikali.

“Natoa masaa 24 kwa  waliovamia shamba la mwekezaji kua wameondoka, wasipofanya hivyo wataona kama serikali hii ni dhaifu au siyo dhaifu kama walivyokua wakitamba kua mpaka wasaini kwa dole gumba la mguu.’’Alisema Msafiri

Aidha mkuu huyo amewaonya wananchi ambao wanaowasawishi  watu kutoka mikoa mingine wenye uwezo wa kifedha kwa ajili ya kuja kuvamia kuacha tabia hiyo mara moja vinginevyo wataunganishwa na wavamizi wanaokuja na kuwasweka ndani.

“Kama mnafikiri serikali haipo endeleeni  kuvamia na kuzigeuza mahakama kua kichaka cha kujificha, awamu hii nitawafunga katika gereza la Babati na hamtatoka kabisa ili mtambue hakuna serikali dhaifu duniani.’’Alisema

Msafiri alisema serikali haitakua tayari kuwavumilia wavamizi  wa shamba la mwekezaji kwa Halmashauri inapata mapato yake ambayo yanawasaidia kuendesha  Halmashauri.

Licha ya mkuu huyo kuwapiga marufuku watu wanaovamia shamba la mwekezaji amemwagiza mwekezaji  wa Ngano Limited Rilash Kalainya  kuhakikisha  analilima shamba alilopewa na serikali ili wananchi  wakaliona alilimwi wakawa na tamaa.

“Kuanzia mwaka huu tutafanya tathimini ya eneo ambalo unalitumia ili kuona kama unalitumia kweli na mwaka kesho hivyo hivyo alafu baada ya hapo tutaandika taarifa na kuituma serikali kuu uendelee kuwepo au lirudishwe      mikononi mwa serikali.’’Alisisitiza

Naye mkurugenzi mtendaji wa  Halmashauri ya  Hanan’g  Braison Kibasa alimtaka mwekezaji huyo kuitendea haki ardhi aliyopewa  ili wananchi wasione kua kuna ardhi ambayo inabaki bila kutumiwa na hatimaye kuvamia.

Pia meneja wa shamba la Ngano Limited Rilash Kalainya aliishukru serikali kwa  kuja eneo hilo  ambalo lilivamiwa na kuaribu vifaa vyake  ili kuweza kumpa msimamo wa kumfanya  aweze kuendelea kuwekeza hapa nchini.

Kalainya alisema kuharibiwa kwa vifaa vyake kumemsababishia hasara ya zaidi ya shilingi mil. 250 ambapo amesema atakata tama ataendelea kupambana kwa kua serikali kumpa ushirikiano kupitia ushauri na vyombo vya ulinzi na usalama.



Kwa upande wake Shedrack Majengo alisema  wavamizi walikuja kijijini hapo watimuliwe kwa kuwa hawana msaada wowote katika kijiji chao na serikali kwa ujumla lakini mwekezaji huyo anawasaidia kutoa huduma za jamii ikiwemo kusaidia ujenzi wa shule na zahanati.

Maoni