Mtunzi wa Kitabu cha kwanini niko hapa Kiteto, achangia hospitali..

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magessa, na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya, Tamimu Kamboka, wakiwa na mtunzi wa kitabu cha kwanini niko hapa..Samwel Maphie muda mfupi baada ya kukabidhiwa Tsh mil moja (1,000,000)
40% ya mauzo ya kitabu hicho, yaliyoelekezwa kusaidia sekta ya afya Kiteto..

 Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magessa, akimkabidhi mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya, Tamimu Kambona mil moja 1,000,000.mauzo ya kitabu cha kwanini niko hapa..
 Mtunzi wa kitabu cha kwanini niko hapa akimsalimia Mkurugenzi mtendaji wa halamshaur ia wilaya ya Kiteto, Tamimu Kambona..

Nasson Kikando mwenyekiti wa kamati ya kitabu cha kwanini niko hapa..
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magessa..
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Tamimu Kambona..


 Na. MOHAMED HAMAD
Ndoto ya mtunzi wa kitabu cha kwanini niko hapa, Bw. Samwel Maphie, imetimia baada ya kutoa 40% ya mapato ya kitabu hicho aliyoahidi wakati wa uzuduzi..

Tukio la kukabidhi kiasi hicho mil 1,000,000, lilishughudiwa na wadau mbalimbali wilayani Kiteto ambapo mwenyekiti wa kamati ya kitabu hicho Nasson Kikando, alimkabidhi mkuu wa Wilaya, Tumaini Magessa, ambaye naye alimkabidhi mkurugenzi mtendaji, Tamimu Kambona, ambapo naye alimkabidhi mganga mfawidhi Dr. Madama..ili ziweze kusaidia katika sekta hiyo..


kwa hisani ya mwanganamatukio..

Maoni