Jitihada za mkurugenzi Kiteto ziungwe mkono.

Tamimu Kambona (DED) Kiteto akiongea katika moja ya kikao .. 



NA. MOHAMED HAMAD.
NIMPONGEZE Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto, Tamimu Kambona, kwa kuonyesha uwezo wa kiutendaji, katika kusimamia miradi ya maendeleo sambamba na kupunguza mang’unguniko ya wananchi.

Hali hiyo imewapa wananchi matumaini makubwa kwa mkurugenzi huyo, hasa alipoweka kambi vijiji vya Sunya na Kijungu kusimamia miradi ya ujenzi kwa lengo la kufikia malengo tarajiwa.

Kambona aliteuliwe miezi 18 iliyopita kushika wadhifa huo baada ya kuteuliwa na Rais Dr John Magufuli, akitokea Mtwara kama afisa elimu,na  Wilaya Kiteto ni ya kwanza kuhudumu katika wazifa huo.

Kiteto ilionekana eneo la wapiga dili kwa baadhi ya watumishi wa Serikali hasa katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, hali iliyofanya wananchi kutowaamini viongozi wao huku wakiomba Serikali kuwabadilishiwa viongozi.

Kambona alianza kusimamia miradi ya ujenzi, ambapo awali ilionekana maeneo mengine yakilalamikiwa na wananchi kwa kujengwa chini ya kiwango huku kukiwa hakuna hatua dhidi ya wasimamizi hao.

Miongoni mwa majengo bora yaliyompa sifa mkurugenzi huyo ni ujenzi wa nyumba moja ya walimu inayotumiwa na familia sita kata ya Sunya ya thamani ya mil 150, madarasa nane Vijiji vya Kijungu na Sunya pamoja na matundu 24 ya vyoo katika vijiji hivyo.

Kambona amesimamia ujenzi wa uzio wa hospitali ya wilaya ya Kiteto wa thamani ya mil 37, pamoja na ukarabati wa soko la wilaya, ambalo awali liliungua moto kwa zaidi ya miaka minne iliyopita 2015.

Halmashauri ya wilaya inauwezo kuhudumia wananchi wake maji safi na salama kwa 36% ya sasa ambapo kwa jitihada sa zaza za kuchimbwa visima 21 katika maeneo mbalimbali kuongeza kiwano na kufikia 50% ifikapo mwezi wa tatu mwaka huu.

Hatua iliyofikiwa katika jitihada hizo ni kutengeneza miundombinu ya maji ambapo wakandarasi wanaendelea na usanifu huku msimamizi mkuu akiwa mkurugenzi huyo ambao hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti alimpa sifa kwa utendaji wake wa kazi

Wilaya ya Kiteto haikuwa na shule ya kidato cha sita hivyo Kambona kwa kushirikiana na wananchi hao amefanikiwa kuanzisha shule Mbili za Kiteto Sekondari na Engusero na sasa zimeanza kupokea wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini

Waziri wa Tawala na Serikali za mitaa, Seleman Jafo, mwezi mmoja uliopota akiwa Kiteto alitembelea Sekondari ya Enguseri na kujionea  jitihada hizo na kuahidi kuipa shule hiyo fedha kwaajili ya ujenzi wa mabweni ambapo kwa mujibu wa Kambona alikiri kupokea fedha hizo.

Jitihada hizo Serikali imetoa mil 400 zingine kwaajili ya uboreshaji wa kituo cha afya Sunya ambapo kazi ya ujenzi imeanza kwa lengo la kupunguza manung’uniko ya wananchi katika huduma ya afya.

Ujenzi wa mitaro wa zaidi ya mil 100 mjini Kibaya umekamilika, huku Sekondari ya kata ya Partimbo ukikamilika na kutakiwa kuanza kupokea wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018


Kimsingi waswahili wanasema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni..kauli hii naiunga mkono na hasa nikipongeza Serikali kwa kuonyesha imani kwa mkurugenzi huyo kwa kutoa fedha nyingi katika miradi ya maendeleo ya wananchi Kiteto.

Mwisho.


Maoni