Waziri Nyongo:Amani idumishwe migodini..


Naibu Waziri Akiwahutubia wachimbaji wadogo..


Naibu Waziri Stanslaus Nyongo Angalia Moja Ya Mashimo Ya Uchimbaji Madini Ya Dhahabu..

Wachimbaji wadogo walijitokeza kumskiliza Naibu waziri..

Wachimbaji wadogo walijitokeza kumskiliza Naibu waziri..






WAZIRI wa madini, Stanslaus Nyongo, amewata wachimbaji wadogo wa mgodi wa Nyakafulu uliopo wilayani  Mbogwe mkoani Geita kudumisha amani na utulivu pamoja na usafi wa mazingira ili kuepukana na magojwa ya mlipuko.

Alisema iwapo kukatokae magonjwa ya mlipuko kama  kipindupindu, mgodi huo utafungwa ili kunusuru maisha ya wananchi kutokana na kushindwa kwao kuzingatia usafi katika maeneo hayo ya mgodi.

Hata hivyo aliwataka wachimbaji hao kuzigatia sheria na taratibu za nchi akisema kila mtu achimbe kwa kuzingatia taratibu na sheria kwani hakuna mwenye leseni ya eneo hilo, hivyo haitaji kusikia mtu akinyanyaswa wala kudhulumiwa.

“Mpo hapa  kwasababu ya kauli ya Mh. Rais wa Jamuhuri  ya muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Makufuli, lakini vilevile akisikia kwamba hapa hakuna  amani na sio wasafi  mimi nitatoa amri ya kufunga mgodi huu kwani wizara yangu ndio inahusika  kutoa leseni hivyo pamoja na hayo  yote amani itawale”alisema Naibu waziri.

Aidha  aliwakumbusha kulipa kodi ili waweze kuchimba kwa kufata  taratibu, sheria, na kanuni za nchi bila kubugudhiwa na mtu yoyote na wangawane kwa utaratibu bila kudhulumiana kwa sababu sehemu wanayochimba kuna leseni ya mtu kwaiyo wachimbe kwa kuweka akiba ili na wao baadae wakate leseni zao za uchimbaji.

‘’Wachimbaji mmekuwa na tabia ya kula bata na kuhonga pesa zote mnapouza madini acheni tabia hiyo  wekeni akiba mkate leseni zenu za uchimbaji, ili muweze kutambulika kisheria” alisema Waziri

Pia aliunda kamati itakayokuwa chini ya mkuu wa wilaya ya Buselesele, ambayo itasimamia  suala la kugawana asilimia ambapo kwa upande wa wasimamizi wa mgodi huo Isanja badugu watakuwa wawili watu wawili kutoka kwa wachimbaji na watu wengine wawili kutoka kwa wenye mashamba wachanguane wapange namna ya kugawana asilimia kwa amani.

Aidha wachimbaji hao walimuomba Naibu waziri wa madini kuwasaidia kupata leseni ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira yao na vitendea kazi kwasababu wamekuwa wakitumia njia za asili katika kufanya shughuli zao za uchimbaji.

Machimbo hayo Nyakafu  ambayo yanakadiliwa kuwa na wachimbaji elfu mbili kutoka sehemu mbalimbali ambapo swala usafi wa limekuwa ni changamoto kwa kukosekana vyoo na maji safi.

MWISHO.

Maoni