DC Same aendelea kuchapa kazi

Ilikuwa ni ziara ya Kikazi kata ya Bendera Wilaya ya Same.kama ilivyo desturi ya DC wa Same kila jumatatu na Alhamisi kuwa  ni siku za kuenda kwa wananchi.

🔸Ashirikiana Na wananchi kusafisha Barabara.

🔸Akaa Na Viongozi ( WDC ) Na kuwaasa kutowachelewesha wananchi kwenye maendeleo.

🔸Asikiliza kero za wananchi - mkutano
wa hadhara Na kutoka mujibu ya kero

🔸 Aagiza wataalamu kumpa majawabu ndani ya wiki mbili Juu ya kero kubwa ya mgawanyo wa Maji ya umwagiliaji.

🔸Awakumbusha wananchi kushika leseni za madini Na kuanza kuchimba Gypsum. Kwani ina ubora kuliko maeneo mengi.

🔸Aagiza Kijiji kutenga eneo lenye madini hayo kwa ajili ya vijana.

🔸Aahidi kuwaagiza idara ya madini kuja kuwapa elimu wananchi Juu ya taratibu za kupata leseni Na uchimbaji.

🔳Atembelea shule Na kukutana Na tatizo la wanafunzi kubakwa.

🔳Akasirishwa Na kuondoka Na muhusika. Na watoto wanne wa kike walihohusika.

🔳Aagiza Polisi kufungua kesi haraka. Aagiza mashahidi kutoa ushirikiano.

Mkuu huyo wa Wilaya Mh. Rosemary Senyamule aliongozana Na wataalamu toka halmashauri Tar. 12/03/2018

Maoni