Same wajipanga kuacha matumizi ya kuni na mkaa

NGO ya VOEWOF  yadhamiria kuimarisha matumizi ya nishati mbadala Wilayani Same..

Katika kikao kilichofanyika Tar 20/03/2018. Wadau wa mazingira walieleza sababu zinazopelekea watu kutochangamkia nishati mbadala pamoja na juhudi za serikali na wadau kuhimiza matumizi yake.

Baadhi ya sababu zinazotajwa ni:-
💡Kutopatikana nishati hiyo vijiji Mf. gas
💡Gharama kubwa ya nishati mbadala, pia kodi katika bidhaa hizo.
💡Mazoea na utamaduni
Ambapo nishati ya kutumia Mkaa na kuni vinapelekea uharibifu mkubwa wa mazingira na upungufu wa maji.

💡Wadau wakubaliana kuongeza matumizi, kubuni na kuanzisha nishati mbadala yenye gharama nafuu,
💡kuendelea kuelimisha juu ya athari ya mazingira na uwepo wa nishati mbadala.
💡Kuhimiza matumizi ya "interlocking block" badala ya tofari za kuchoma.
💡Kusimamia sheria.

💡Shirika la VOEWOF linalofanya kazi chini ya CARE International linafanya kazi na vikundi vya wanawake. 
💡limewezesha majiko ya gas zaidi ya 300 kutumika vijijini.
💡Limepania kuanzisha viwanda vya kutengeneza nishati mbadala kwa kutumia taka.
💡Wilaya yaahidi kutoa eneo, kutoa mikopo kwa vikundi hivyo na kutumia miti inayooteshwa na vikundi hivyo.

Kikao hicho pia kimewashirikisha DC wa Same, wataalamu toka ofisi ya RC Kilimanjaro na halmashauri ya Same, TBS, wanazuoni toka SUA, TRA, wauzaji wa nishati mbadala, wanavikundi hao na vyombo vya habari.

DC Same alipongeza na kuwashukuru VOEWOF Na wadau wengine jinsi wanavyoshiriki kuibadilisha Same, kila mmoja kwenye nyanja yake. Alikiri kuwa kwa kasi hii; Wilaya ya Same itafikia malengo yake ya kubadili mazingira ya Same.

" Same is not same"

Maoni