DC ashusha bei ya Nyama Mbulu

DC Mbulu ashusha bei  ya nyama.

Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara Be. Chelestino Mofuga ameagiza wafanya biashara ya nyama kuuza kilo moja sh 6000 kutoka 7000.

Hatua hiyo imetokana na  kukutana na wafanyabiashara  hao wa nyama na kujadili changamoto wanachokabiliana wafanyabiashara hao

Kikao hicho kilifanyika katika  ukumbi wa community center katika  Halmashauri ya mji wa Mbulu  Juni 6 mwaka huu.

Mkuu wa wilaya mwanzo aliwataka wafanyabiashara hao kutoa sababu za msingi zinazowafanya bei ya nyama Mbulu iwe  juu kuliko sehemu nyingine bila majibu ya msingi.

Kutokana na amri hiyo wafanyabiashara hao akiwemo Philipo Shauri alisema bei  ya nyama iko juu kwa sababu Ng'ombe kwa wilaya ya Mbulu hawapatikani kama ilivyodhaniwa na wengi.

Wakati wa mvutano huo wafanyabiashara hao hawakuonyesha utayari wa kupunguza bei  hiyo kutoka 7000/ baada ya Mkuu wa wilaya kuonyesha msimamo wake bei  ilipendekezwa kuwa iwe  6000/ kwa kg moja.

Wafanyabiashara hao waliomba wiki moja kabla ya kushusha bei  ili wajiandae kwa mabadiliko mpya ya bei  na Mkuu wa Wilaya akawapa siku  saba kutoka tarehe 6.6.2018 hadi  13.06.2018.

Mkuu huyo wa Wilaya Bw. Mofuga  alihitimisha kwa kuwataka wafanyabiashara hao kutii makubaliano hayo yaliyoafikiwa na pande zote mbili.

Maoni