WAKULIMA KITETO WAENDELEA KUPOKEA KICHAPO CHA WAFUGAJI

Karibuni kwenye Blogu yangu upate Matukio Na mambo mbalimbali kila wakati







Aliyelala ni mmoja wa wahanga wa migogoro ya ardhi Bw. Sangali Athumani aliyekatwa mapanga na baadaye kufariki Dunia akiwa Hospitali ya Muhimbili Dar eS Salaam.

Bw. Sangali Athumani wa Kiteto Manyara akiwa amekaa kabla ya kifo chake kilichosababishwa na watu wanaodaiwa kuwa jamii ya kifugaji wamasai kumkata mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake

DIWANI AFARIKI KITETO AKICHUNGA MIFUNGO:

Aliyekuwa Diwani wa kata ya Lolela Kone Lembile enzi ya uhai wake akiwasilisha kazi za vikundi katika moja ya Semina mjini Kibaya Picha na Mohd Hamad:


Marehemu Lembile alifariki wakati akikimbizwa kwenda Hospitali ya Wilaya ya Kiteto baada ya kuanguka ghafla akichunga mifugo yake

Kwa mujubu wa Daktari aliyeweza kuuona mwili na kuuchunguza alisema kifi cha Marehemu Lembile kimetokana na presha ya kushuka 

Tatizo hilo limemkumba kwa muda mrefu hadi umauti ulipomkuta na kwamba atazikwa katika kata ya Lolela nyumbani kwake siku ya jumatatu.  
XXXXXXXXXXX
 PICHA YA PAMOJA KWA WANACHAMA WA SHIRIKA LA MWANASATU LINALOFANYA KAZI WILAYANI KITETO


Kiteto hatutashiriki uchaguzi mkuu 2015

Na Mohamed Hamad
BAADHI ya wananchi wilayani Kiteto Mkoani Manyara wametishia kutoshiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za Serikali kushindwa kuwatambua kwa kuwakwamua kiuchumi hali inayofafanya waendelee kuwa maskini

Wakizungumza hayo kwenye mkutano wa katiba ulioandaliwa na Shirika lisilokuwa la Kiserikali la MWANASATO linalo jishughulisha na utetezi wa wagane na wajane pamoja na makundi maalumu wamesema hawako tayari kushiriki uchaguzi mpaka Serikali itakapoona umuhimu wao

“Hatuwezi kuitwa makundi madogo madogo ndani ya jamii wakati tunashiriki kikamilifu kuendeleza nchi hii kwa kufanya kazi za kuliendeleza taifa lakini mwisho wa siku kupitia IBARA ya 45 ya rasimu ya katiba ya mwaka 2013 Serikali iseme wakulima na wafugaji  ni makundi madogo ambao watatengewa ardhi kwaajili ya kujipatia risiki”

Wakifafanua Ibara hii wajumbe hao walisema mameno haya yanaundhi na yanadhalilisha watanzania kuwa wao Serikali itawapatia sehemi ya ardhi kwaajili ya kujipatia riziki na sio kuwajengea uwezo kuondokana na umaskini wa kipato

Akizungumza hayo Hasani Konki (mshiriki) alisema kama katiba ijayo itawatambua wakulima na wafugaji na kuweka utaratibu maalumu wa kuendesha maisha yao pamoja na kujengewa uwezo wa kuondokana na umaskiti watashiriki uchaguzi la sivyo hawatakuwa tayarai

Kwa upande wake Kemaa Lenyirai (mfugaji) alipendekeza katiba ijayo itambue mchango wa viongozi wa mila ambao wamekuwa msaada mkubwa ndani ya jamii kwa kutatua matatuzo mbalimbali yanayowahusu

“Kwa mfano jamii ya kifuagaji hatuna sababu ya kwenda mahakamani tunapohitilafiana badala yake tunawatumia  viongozi wa mila kutatua matatizo yetu kuepuka usumbufu ambao tunauona watu wanapoenda mahakamani ambako rushwa imekithiri kupata haki”

Kemaa alisema kama Katiba ijayo itawatambua viongozi wa mila ndani ya jamii ni wazi kuwa matatizo ndani ya jamii yataisha tofauti na ilivyo sasa kwa kila lalamiko linalowasilishwa mahakamani kuna ucheleweshaji wa kesi lakini pia kukithiri rushwa

Naye Waziri Godah (mwanasheria) wilayani humo alilaani kitendo cha tabia za wajumbe wa mabaraza ya katiba kufanya mzaha katika uchangiaji wa maoni ya katiba mpya akisema wengi wao wanaingiza mzaha, ushabiki pamoja na dharau

Alisema kama zoezi hilo litaendelea kuchangiwa kishabiki katiba ijayo haitajibu matatizo ya wananchi na badala yake itakuwa na mambo machache ambayo itawalazimu watawala kufanya marekebisha tena kwa siku za usoni

Katika ufafanuzi Godah alisema wapo watu wanaofika kwenye mkutano kwaajili ya agenda moja tu ya kupiga kura kutaka aina ya Serikali lakini wamekuwa hawana hoja za msingi kutetea hoja zao na kuonekana kuwa wameagizwa na watu fulani

Hata hivyo katika zoezi la kupiga kura juu ya kuhitaji aina gani ya Serikali wanayotaka, idadi kubwa ya wajumbe hao zaidi ya 80% waalitaka Serikali mbili kwa madai kuwa Nchi ni maskini haiwezi kuendesha serikali tatu

Mratibu wa shirika hilo Godwin Nagor akizungumza na BLOG hii baada ya  mkutano huo wa katiba alisema wamefikia wananchi hao kutaka wachangie mapendekezo ya katiba mpya baada ya kutofikiwa na Serikali

“Shirika tumafanya kazi ya utetezi wa wagane na wajane pamoja na makundi mengine hivyo baada ya Serikali kushindwa kuwafikia kama yalivyo makundi mengine Shirika tukaona kuna haja ya kuwashirikisha kutoa maoni yao”

Alisema ni historia ya pekee toka kupata uhuru kwa mara ya kwanza Watanzania wanashiriki kuunda katiba yao tofauti na katiba iiyopita ambazo ilibeba mawazo ya watu wachache na kusasabisha manunguniko makubwa ndani ya jamii

Mwisho
   

Maoni