MOTO WASABABISHA HASARA YA ZAIDI YA MIL 150 KITETO

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bi Jane Mutagurwa akionyeshwa jinsi moto ulivyoteketeza maduka soko kuu ya Kiteto


Maduka kumi yateketea kwa moto Kiteto
Mohamed Hamad Manyara
ZAIDI ya maduka kumi ya wafanya biashara wa soko kuu la kiteto Mkoani Manyara yameteketea  kwa moto ulioibuka usiku wa kuamkia Aug 23 mwaka huu na kusababisha hasara ambayo thamani halisi haijafahamika kwa haraka

Moto huo ulianza saa nane za usiku ambapo chanzo chake kinadaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme katika moja ya maduka hayo ambayo yameteketea vibaya baada ya watu waliofika kushindwa kuudhibiti moto huo

Kwa mujibu wa Ofisa mtendaji wa kijiji cha Kibaya Fatuma Ngao amedai kuwa vitu vilivyoteketea ni pamoja na maduka hayo kumi nyaraka mbalimbali za Serikali ofisi ya kijiji pamoja na baraza la ardhi la kata
Baadhi ya mashughuda watukio hili wamezungumza na kipindi hiki na hapa wanasema.. ….

Amsema kuwa nyaraka hizo ni pamoja na vitabu mbalimbali ambazo zilitumika kama kumbukumbu za Serikali, viti na meza ambazo zilitumika katika kuihudumia jamii ya Kibaya na vitongoji vyake

Ngao alisema alipata taarifa hizo kupitia matangazo yaliyotolewa kwenye moja ya msikiti mkuu mjini hapo ya kuwaomba wananchi hao ili waweze kufika kuokoa mali zilizokuwa zinateketea katika soko hilo

Alisema baada ya wananchi hao kufika walishindwa kuudhibiti moto huo ulioteketeza maduka yote kwa kuwa hawakuwa na vitendea kazi na kwamba wananchi walilazimika kuangalia hadi ulipoisha

“Wapo waliojaribu kutafuta maji kutaka kuzima moto huo lakini walishindwa nguvu na kuutazama tu hadi TANESCO walipofika na kuzima umeme mji mzima usiku huo lakini hata hivyo aijasaidia”alisema Ngao

Shuhuda wa tukio hilo Adiu Ally (mfanya) aliliambia MTANZANIA kuwa baada ya kufika hapo alikuta kundi kubwa la vibaka wakipora mali mbalimbali sokoni huku wengine wakijaribu kuzima moto huo

“Nilikimbilia dukani kwangu na kusimama mlangoni ili vibaka hao wasiibe duka langu lakini maeneo mengine maduka yaliungua hakuna kilichookolewa huku baadhi watu wakiendelea kupora vitu mbalimbali vya sokoni”alisema

Katika hatua hiyo mmoja wa Askari wa kituo cha Polisi kibaya ambaye hakutaka kutajwa majina yake alisema kuwa duka lake hawakuweza kuambulia chochote baada ya kuteketea kwa moto huo

Kamanda wa Polisi mkoani Mnayara Akili Mpwapwa alikiri kuibuka moto huo na kusema kuwa Jesi la Polisi linaendelea na uchunguzi kutaka kubaini chanzo cha moto huo pamoja na thamani halisi ya hasara iliyojitokeza

Mwisho


Maoni