MTOTO AOKOTWA AMEKUFA KISIMANI


Mtoto aokotwa amekufa kisimani

Na. Mohamed Hamad
MTOTO aliyefahamika kwa jina la Mathias Gwaatema Barani (8) mkazi wa Kijiji cha Endamanag Kata ya Nar Wilayani Babati Mkoani Manyara, ameokotwa akiwa amefariki kwenye kisima cha maji kilichochimbwa kwa mikono

Awali mtoto huyo alitumwa kwenda kuchunga mifugo yao na wazazi wake porini na ilipofika jioni hakuweza kurejea ndipo wazazi wakatoa taarifa kwa majirani na kuanza safari ya kumtafuta
Akizungumza na BLOG Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nar Bw.Phillipo Moe alisema alipata taarifa kutoka kwa wanajamii hao na baadaye kujulisha Jeshi la Polisi Wilayani Babati kwaajili ya hatua zaidi

“Binafsi baada ya kupata taarifa niliweza kujiridhisha na kutoa taarifa Polisi ambapo nao walifika asubuhi ya Leo (jana) na kuelekea eneo la Tukio ambapo tulimkuta mtoto akielea kwenye kisima cha maji”
Alisema hatua ya kuopoa mwili huo ilifanyika na mwili kukabidhiwa kwa wazazi wake kwaajili ya mazishi huku Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi wa tukio hilo

Ofisa huyo alisema mtoto huyo alitumwa na wazazi wake kwenda kuchuga mifugo na kuongeza kuwa mifugo ilipatikana siku hiyo na kurejeshwa nyumbani ikiwe kwenye shamba la mmoja wa wana kijijini hicho
Akizungumzia mazingira ya kifo hicho Mtendaji huyo wa Kata alisema kuwa hakuna anae hisi chochote juu ya kifo hicho akisema kuwa huenda mtoto huyo alitumbukia mwenyewe akitaka kunywa maji

“Tunachohisi hadi sasa ni kwamba kwakuwa mtoto huyo alikuwa ni mdogo labda alishikwa na kiu ya maji na kutaka kuchota maji ili anywe, kutokana na hatua hizo huenda alishindwa na kudumbukia ndani”alisema Ofisa huyo

Hata hivyo BLOG ilitaka kujua kama ni kawaida kwa watoto wadogo kuchunga mifugo katika eneo hilo na kuelezwa kuwa imekuwa ni mazoea kwa wafugaji kutuma watoto wadogo kwenda kuchunga mifugo

Alisema Serikali imepiga kelele juu ya jamii ya kifugaji kuacha kuwatumia watoto wadogo kuchunga mifugo bila mafanikio na kuongeza kuwa tatizo lililopo na ubutu wa sheria ambapo mtu akikutwa na kosa mahakamani hupewa adhabu ndogo

Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara Akili Mpwapwa amekiri kutokea tukio hilo na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi ninaendelea kufanya uchunguzi juu ya kifo cha mtoto huyo

Mwisho

Maoni