Mwanafunzi wa Kiteto Sec anusurika kifo kwa kuchomwa na kifu wivu wa mapenzi Kiteto


    Mwanafunzi Bestina Mchunguzi wa Kiteto Sekondari akiwa katika Hospitali ya 
    Kiteto baada ya kuchomwa kisu tumboni kwa tuhuma za kugombea wanaume



Mwanafunzi anusurika kifo kwa tuhuma za mapenzi
·          
  •       Achomwa kisu tumboni,alazwa Hospitali ya Kiteto
Na Mohamed Hamad MANYARA
MWANAFUNZI mmoja wa shule ya Sekondari ya Kiteto Mkoani Manyara Bestina Mchunguzi, amelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Kiteto baada ya kuchomwa kisu na mwanafunzi mwenzake kwa tuhuma za wivu wa kimapenzi

Akiongea kwa taabu akiwa amelazwa katika Hospitali hiyo Bestina alisema hali yake bado haijatengemaa kutokana na majeraha aliyopata ya kuchomwa kisu tumboni pamoja na kukatwa sehemu ya mkono wake

Tukio hilo limetokwa Aug 23 mwaka huu mjini Kibaya katika viwanja vya shule ya msingi Kibaya ambapo wanafunzi Mwajuma Ally alimchoma mwenzake kisu tumboni na kumsababishia kutokwa na damu nyingi hatimaye kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto

Alisema siku hiyo alikuwa mjini Kibaya baada ya kutoka shule na ndipo walipokutana na mwenzake huyo aliyekuwa na kisu hatimaye kumchoma tumboni na kuanguka chini

Kwa mujibu wa baadhi ya wanafuzni waliozungumza na MTANZANIA walieleza kuwa chanzo cha ugonvi huo ni kugombea mabwana ambapo awali kabla ya tukio walipigana shuleni na waliporejea nyumbani wakaendelea na ugomvi huo

“Walipigana wakiwa shuleni na walipokutana Mwajuma alimwambia mwenzake kuwa kwanini ulimitoa damu shuleni akasema leo nitakufanya nitakavyo, akamchoma kisu tumboni na alipong’ang’ania akakatwa tena mkononi”alisema mmoja wa wanafunzi hao

Akisisitiza kauli yake hiyo Fatuma Kiteka (mwanafunzi) alisema kuwa vitendo hivyo vimekithiri shuleni hapo hasa kwa vijana wa kiume kutoka mitaani kuwa na mahusiana ya kimapenzi na zaidi ya mwanamke mmoja

“Tunayaona sana hapa shuleni waalimu wamekuwa wakipiga sana kelele juu ya vitendo hivi lakini wamekuwa wakipuuzwa na leo hii haya ndiyo madhara yake kwani imekuwa ni mazoea na kama fasheni mwanafunzi kuwa na bwana shuleni”alisema mwanafunzi huyo

Naye Neema Magimbi (mwanafunzi) alitaja sababu za wanafunzi kujikita katia vitendo hivyo ni kuendekeza starehe shuleni na wengine kufanya kazi hizo kama moja ya kujipatia vipato wanapokuwa shuleni

“Wapo wanaofanya kazi hii ili waweze kuishi lakini pia wapo wanaofanya kwa hulka zao sasa hili sina jibu sana ila tatizo hili ni kubwa linahitaji nguvu ya ziada hapo shuleni kwa kila mara yanapojitokeza huishia hewani”alisisitiza Neema

Kwa mujibu wa mmoja wa madaktari katika Hospitali ya wilaya ya Kiteto ambaye hakutaka kutajwa majina yake alisema hali ya majeruhi huo inaanza kutengamaa baada ya kusafishwa kidona na kuondeza kuwa walilazimika kumpiga opereshen ili kumsafisha

Alisema kuwa katika hatua hizo mwanafunzi hiyo amekazimika kuongezewa damu chupa mbili baada ya kuoneka kuwa na upungufu na katika hali ya kumwokoa wakalazimika kumwongezea alisema daktari huyo

Uchunguzi uliofanya na MTANZANIA umebaini kuwepo kwa biashara za ngono kwa wanafunzi hao ambapo mimba na utoro vimetajwa kutokea katika sekondari hiyo hali inayodaiwa kuwa huwa inazibitiwa mara kwa mara

Akizungumza hayo mwalimu mkuu wa Sekondari hiyo aliyefahamika kwa jina moja la Kimaro amekiri kutokea vitendo hivyo na kuongeza kuwa uongozi wa shule hiyo umekuwa macho kuvizibiti na kuongeza hali na majeruhi huyo inaendelea vizuri

Kuhusu mwanafunzi Mwajuma Ally Mussa kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Wilayani Kiteto kwa Tuhuma za kumchoma mwenzake na kumsababishia maumivu makali na yuko katika mahabusu ya gereza la Kiteto


    Mwanafunzi Mwajuma Ally Musa anayetuhumiwa kumchoma kisu mwanafunzi mwenzake kwa tuhuma      za   kugombea wanaume

Mwisho

Maoni