VIONGOZI:WANANCHI ACHENI KULALAMIKA VIJIWENI



Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Minge Lemalali akisisitiza Jambo.


Wananchi acheni kulalamikia vijiweni

Na. Mohamed Hamad
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Mainge Lemalali amewataka wananchi wilayani humo kuacha utamaduni wa kulalamikia vijiweni badala yake waende ofisi husika kueleza kero zao

Malalamiko hayo yanatokana na kutoridhika na huduma za jamii zinazotolewa na Serikali hali inayowafanya wananchi hao kuwa na manung’uniko na kulalama vijiweni bila kupata ufumbuzi

Akizungumza kwenye kongamano la Jinsia lililoandaliwa na Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (KCS Forum) Wilayani Kiteto Mwenyekiti huyo alikiri wananchi kutopata huduma za Jamii kwa kiwango stahili

“Wananchi acheni kulalamikia vijiweni kwenye kahawa njooni ofisini tuongee matatizo yetu ili tuyatafutie ufumbuzi, kwani kuzungumza vijiweni hakusaidii kufumbua tatizo”alisema Mainge

Alisema yapo matatizo mengi ya ardhi katika mirathi, huduma za maji, Afya, kuwa kuna changamoto nyingi zanahitaji kuzungumza kwenye vikao na hata ofisini na sio vijiweni kama ilivyo sasa

Aidha Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa ili wananchi waweze kupata maendeleo lazima kuwepo kwa maafikiano ya viongozi katika kujadili na kufikia mwafaka mambo yanayowahusu

Kwa upande wake Ramadhani Machaku (Zoa) akizungumza na BLOG kuhusu malalamiko ya wananchi alisema kuwa wananchi wamekosa imani na kukata tamaa kwa viongozi wao kuwa wanaweza kuwasaidia

Alisema kila mara wamekuwa wakiilalamikia Serikali yao juu ya huduma mbovu za Afya,Elimu, na hata maji viongozi wanajua lakini wamejifanya kuwa sehemu ya watu wasiojua kinachoendelea

“Hata huku kuzungumzia vijiweni ni matokeo ya kutoshughulikiwa malalamiko yetu na huko tunajasirishana ili kutengeneza uelewa wa pamoja mwisho wa siku tuwe na maamuzi pamoja”

Alisema tatizo la wananchi ni Serikali iliyopo madarakani kuwahujumu, hivyo hakuna kiongozi asiyejua hitaji lao na hata kama viongozi wanataka kuzungumza na wananchi ni kujikosha alisema Mwananchi huyo

Ameitaka Serikali kuacha kuruka kimanga juu ya kutojua mahitaji ya wananchi hasa akisema kuwa,viongozi walipokuwa wanahitaji kuingia madarakani waliyajua matatizo ya wananchi na sio vinginevyo

Naye mratibu wa mtandao wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikaili KCS Forum Nemes Iria akizungumza kwenye kongamano hilo la Jinsia alisema lengo la mashirika ya umma ni kuisaidia Serikali katika majukumu yake

Alisema yapo matatizo mengi yanayo wakabili wananchi akidai kuwa mengi ni yakisera zaidi ambayo wakati mwingine Serikali inatakiwa kurekebisha baadhi ya Sheria zinazowakandamiza wananchi



Mmoja wa wanajamii ya kifgaji wmasai akijaribi kupitia Rasimu ya katiba

Maoni