MAUAJI TA KINYAMA YAZIDI KUJITOKEZA KITETO

MAUAJI KITETO YAZIDI KUJITOKEZA SERIKALI VUNJENI UKIMYA

Wakulima 10 wauawa kwa kuchomwa mikuki Kiteto
·          
-Ni Mwendelezo wa mauaji Wilayani kiteto
·         OCD awahi eneo la tukio kuzima mapigano
·         RC Manyara akiri madudu Kiteto

Na. MOHAMED HAMAD
WAKULIMA sita wa kijiji cha Namelock Kata ya Namelock Wilayani Kiteto Mkoani Manyara wameuawa kwa kuchomwa mikuki sehemu mbalimbali za miili yao baada ya kuvamiwa kwenye makazi yao na kundi kubwa la wafugaji (wamasai) wakiwa na silaha za moto bunduki, mikuki, sime, na marungu

Vifo hivi ni mwendelezo wa mauaji yanayofanywa na jamii ya kifugaji (wamasai) ikielezwa kuwa miili mingine iko porini wakilenga kuwaondoa wakulima kwa nguvu baada ya madai yao kuwa Halamshauri imeshindwa kuwatoa wakulima hao katika maeneo yao

Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi Mkoani Manyara Akili Mpwapwa amethibitisha kutokea vifi hivyo akisema miili mingine inayodaiwa kuwa porini inasakwa kutokana na jamii ya wafugaji wamasai kuvamia wakulima katika maeneo yao

“Ni kweli kuna idadi ya watu sita waliopotea maisha na majina yao hayajafahamika mapema kuwa wameuawa na wafugaji katika maeneo ya laitimi wakiwa mshambani huu ni mwendelezo wa migogoro ya ardhi Wilayani Kiteto kati ya wakulima na wafugaji” alisema RPC

“Halmashauri ilituchangisha mamilioni ya fedha kwaajili ya kuwaondoa wakulima, ikiwa zoezi hili likisimamiwa na mkurugenzi kwa kushirikiana na viongozi wa mila wa jamii ya Kimaai ili kupata fedha zitakaosaidia mamlaka inaohusika kuwatoa kwa nguvu kotibroka na (Polisi)”alisema mmoja wa wafugaji

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Eraston Mbwillo Kisioki Mesiaya (mfugaji) Jan 9 alisema wamasai wamechangishwa mamilioni ya fedha na Mkurugenzi kwa madai ya kuwaondoa wakulima, kwa kuwa kazi hiyo haikufanywa na Halamshauri wafugaji wao wameamua kuifanya

Kwa mujibu wa Diwani wa kata ya Sunya Mussa Briton alisema watu wawili wamepoteza maisha na wengine zaidi wamedaiwa kutoonekana kwenye makazi yao baada ya kuvamiwa wakiwa eneo la  Lemenye na Laitimi ambako hufanya shughuli zao za kilimo

Alisema Mauaji hayo ni ya maksudi yanayotekelezwa na jamii ya kifugaji wamasai akidai kuwa, pamoja na kutajwa majina ya baadhi ya watu wanaopanga njama hizi imeshindikana kukamatwa kwa madai kuna mkonno wa kiongozi wa Wilaya anaye wasimamia

“Haiwezekani hata kidogo watu wafanye mauaji na kutajwe wasikamatwe kwa madai eti wanamahusiano na kiongozi wa ngazi ya juu ya juu, jambo hili halikubaliki naomba Serikali ya ngazi ya Taifa kuingilia kati”alisema Beriton

Alisema jamii ya Kifugaji wamasai wamekuwa wakiwavamia wakulima na kuwaaua kisha kukimbilia porini na baada ya muda hurejea na kuwavamia tena akidai kuwa tukio hili ni la nne toa Dec 21 hadi Jan 12 mwaka huu kuwa zaidi ya watu kumi wamepoteza maisha

Kwa upandw wao wakulima wamedai kuwa wako tayari kuuawa ili Serikali iingilie kati wakidai kuwa nayo imechangia kwa kuwagawa wakulima na wafugaji Kiteto kikabila na kuendekeza Rushwa iliyokithiri na kusababisha madhara makubwa

“Serikali inajua kuwa ilifanya nini mpaka sasa mauaji yanatokea watakaobaki wataeleza kilichotuua sisi kwani Serikali ya Kiteto inahusika katika mauaji haya kwani imekula feda za wafugaji na inashindwa kurejesha”Alisema Bakari Maunganya Mkulima

Baadhi ya wananchi Wilayani humo wameutupia lawama uongozi wao wa Wilaya akiwemo Mbunge wao Benedict Ole Nangoro kwa kutoshtuka na mauaji ya kinyama yanayoendelea kujitokeza Jimbo kwake wakisema kuwa huenda anahusika

Akiuliza swali Mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Saidi Mwawa alimtaka Mkuu wa Wilaya ya Kiteto  Martha Umbula kueleza umma kuwa Mbunge wao yuko wapi na kuelezwa ana kazi maalumu aliyopewa na Mh. Rais hivyo asingweza kufika kwenye mkutano huo

Kwa mujibu wa taarifa za uhakika zimeeleza kuwa chanzo za mapigano hayo ni jamii ya kifugaji kuchangishwa fedha na uongozi wa Halmashauri ili waweze kuwaondoa wakulima wapate maeneo ya malisho

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa manyara Eraston Mbwillo amekiri wafugaji kuchangishwa fedha kinyume na taratibu za Kiserikali akisema kuwa atahakikisha kuwa waliohusika na suala hili sheria itafiata mkondo wake

Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri ya Wilaya ya Kiteto Bi. Jane Mutagurwa alikiri kuchanga fedha hizo akidai kuwa waliohusika kuchanga ni jamii ya watu wa Kiteto kwaajili ya kuisaidia Halmashauri kwenye operesheni ya kuwaondoa wakulima katika hifadhi

Mwisho  

Maoni