Halmashauri Kiteto kuburutwa Mahakamani na wakulima


Halamshauri Kiteto kuburutwa Mahakamani
·          
  • Ni baada ya kuvunja makazi ya wakulima

Na. Mohammedi Chumvi
JUMLA ya wakulima 20 wa Kijiji cha Kimana Wilayani Kiteto Mkoani Manyara wameapa kuishitaki Halmshauri ya Wilaya ya Kiteto kwa madai ya kuvunjiwa makazi yao kinyume na sheria na kusababishia hasara ya zaidi ya million thelathini na tano

Makazi ya wakulima hao yalivunjwa kutokana na operesheni maalumu iliyofanywa na Halmashauri aya Wilaya na kudaiwa wakulima waliporwa fedha,simu za mikononi,pamoja na mali mbalimbali za dukani

“Binafsi nyumba yangu ilivunja kulikuwa na duka lililokuwa limesheheni vitu mbalimbali ikiwemo sukaru unga wa ngano n vitu vingine ambapo Askari Polisi na Migambo wakiongozwa na OCD walivamia na kuvunja nyumba pamoja na kuchukua fedha taslimu zaidi ya mili 9 za kulipa vibarua”alisema Vita bado (mkulima)

Katika hatua nyingine mkulima huyo alisema kama kweli kulikuwa na uhalali ya zoezi hilo alipaswa kukamatwa akiwa na vifaa hivyo na kufikishwa mahakamani kwa kuwa siku zote yupo na ameendelea kupata vitisho vya maisha akiwempo humo

Kwa upande wake Mntunte Waziri (mkulima) akizungumza na NIPASHE alisema amesababishiwa hasara ya zaidi ya mil 15 baada ya kikosi hicho kuvamia kwake na kuchoma moto nyumba zake tatu zikiwa na fedha zaidi ya mil 9 zilizokuwa ndani pamoja na vitu mbalimbali zikiwemo nguo na thamani zingine

“Ninachofanya ni kuwasiliana na wezangu ambao kwa pamoja tumeamua kuishitaki 
Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto walioamua kutufilisi ili Sheria ifuate Mkondo wake kwani tumedhalilishwa sana,tumenyanyasika na familia ndani ya nchi yetu kwa ujumla”alisema Mntunte

Naye Ibrahimu Msindo (mkulima) alisema Halamshauri ya Wilaya ya Kiteto inafanya kazi kimila kwa kuamuriwa kufanya kama watakavyo wafugaji akisema kuwa walichanga zaidi ya mil 500 ili kuwatoa wakulima

“Kimana haipo kwenye nakala ya hukumu iliyotaka wakulima na wafugaji waliopo humo waondolewe tena kwa kupewa elimu na sio kuvunjiwa kama walivyofanya Halamshauri sasa hapa lazima tuingie mahakamani”alisema Msingo

Wakati Halmashauri ya Wilaya ikiwa katika Operesheni ya kuwatoa wakulima waliopo kwenye eneo la Hifadhi ya Emboley Murtangos wafugaji wamedaiwa kutumia fursa hiyo kuchunga mifugo yao kwenye ashamba ya wakulima

Akizungumza hayo Bakari Maunganya (Mkulima) alisema jamii ya kifugaji wamasai wamekuwa kama Serikali Wilayani Kiteto akisema Viongozi wa Kiteto wanafanya kama wanavyotaka wafugaji mfano kuwatoa wakulima li wachunge mifugo yao

Hivi karibuni Kisioki Mesiaya (mfugaji) akizungumza mbele ya mkuu wa Mkoa wa Manyara Elaston Mbwillo alisema wafugaji walichangishwa na Uongozi wa Halamshauri ya Kiteto ili waweze kuwapatia maeneo ya kuchungia mifugo yao

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Bi. MARTHA Umbula akizungumza na NIPASHE Ofisini kweke alisema kutokana na zoezi hili hakuna mkulima wala mfugaji aliyopo kwenye eneo la Hifadhi hiyo na kwamba Serikali inatekeleza agizo la Mahakama kuu kuwa eneo hilo pasifanyike shuguli za kibinadamu

Kuhusu mifugo kuchunga  mashamba ya wakulima Mkuu huyo wa Wilaya alisema hata yeye amesikia hilo akisema kitendo hicho ni kosa kwa wafugaji na kuwataka waache kitendo hicho mara moja

Kuhusu kuvunjwa kwa makazi ya baadhi ya wanakijiji wa Kimana alisema kama kweli hawapo kwenye eneo la Emboley Murtangos Serikali itawagharamia hasara iliyopatikana akisema kuwa kweli kuna mpaka uliowekwa mpya na kuongeza eneo hilo akisema upo utaratibu unaoandaliwa

Mwisho   

Maoni