HAYA NI MABAKI YA MIRADI YA PADEP WILAYANI KITETO

Mradi huu wa soko wa Kijiji cha Sunya Wilayani Kiteto umegharimu zaidi ya mil 45 mbali ya michango ya wananchi,mkanarasi ni Kampuni ya KOMBA ambayo ulianza kazi hiyo mapema mara tuu baada ya kukamilika kwa uchaguzi Mkuu

John Komba akiwa katika uchaguzi huo aliapa kuwa kama mradi huo hautakamilika basi afuatwe yeye na kwamba atahakikisha kuwa unakamilika kwakuwa anajua kila kitu katika kampuni hiyo

Toka kumalizika kwa uchaguzi huo Mhe.Komba aliingia mitini hajulikani lini atafika tena Kiteto huku baadhi ya wadadisi wa mambo wakisema huenda akafika wakati mwingine wa Uchaguzi kuombea wenzake kura 

Kwa sasa Soko hilo ni kama linavyoonekana limetelekezwa hakuna wa kulisemea baada ya kila kiongozi kuruka kimanga kuwa hahusiki na ujenzi huo HII NDIO SERIKALI YA TANZANIA BWANA

Maoni