MWANAMKE KITETO KIZIMBANI KWA KUSAMBAZA MADAWA YA KULEVYA


Mwanamke kizimbani kwa madawa ya kulevya Kg 94 Kiteto

NA. MOHAMED HAMAD
Jeshi la Polisi Wilayani Kiteto Mkoani Manayara limekamata shehena ya madawa ya kulevya aina ya mirungi yenye uzito wa Kg 94 zilizokuwa zikisafirishwa kwenye gari aina ya Noah yenye namba za usajili T 817 TJB

Dereva wa gari hilo na watu waliokuwemo walikimbia na kulitelekeza gari hilo eneo Jangwani Kijiji cha Bwagamoyo ambapo Polisi walilichukua na kulihifadhi katika Kituo cha Polisi cha Kiteto kwa uchunguzi zaidi

Chanzo cha uhakika cha habari hizo kimesema shehema hiyo inadaiwa kuwa ililengwa kusambazwa Wilayani Kiteto na baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Chemba (Mjirijo) na Kondoa ambako watuhumiwa hao wanadaiwa kuishi humo

Alisema hadi sasa hakuna anayeshikiliwa kwa kukutwa na shehena hiyo ya madawa ya kulenya na kwamba baada ya upelelelezi kukamilika sheria itafuata mkondo wake kwa wahusika kufikishwa Mahakamani

Kuhusu watuhumiwa kukimbia na kulitelekeza gari hilo chanzo hicho kilisema ni rahisi kumjua miliki wa gari hilo kupitia Ofisi za TRA hivyo kama wahusika hawajajitokeza ndani ya siku saba wataenda TRA ili kumjua mmiliki wa gari hilo

Kwa mujibu wa Sheria imelezwa kuwa mara baada ya kukamatwa kwa madawa hayo huteketezwa ili yasitumike ndani ya jamii kama ilivyokusudiwa na mmiliki kwa kusambazwa kwa watu wanaodaiwa kutumia madawa hayo

Pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa Jeshi la Polisi kuwakamata wahalifu hao wanaofanya biashara  ya madawa ya kulevya na kufikishwa mahakamani kila mara watu hao wameendele kuifanya na kusababisha usumbufu mkubwa kwa Jeshi hilo

Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara Akili Mpwapwa amethibitisha kukamatwa kwa shehena hiyo na kudai kuwa upelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika na watuhumiwa kukamatwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo

Mwisho

Maoni