14 mbaroni kwa tuhuma za mauaji Kiteto
·      
   Yumo aliyekuwa Diwani wa CCM Namelock
·        
 10  wako chini ya uangalizi wa Polisi
·      
   6 bado wanaojiwa na polisi

NA. MOHAMED HAMAD
Jumla ya watu 12 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilayani Kiteto kwa tuhuma za mauaji ya wakulima 10 waliouawa wakiwa katika makazi yao maeno tofauti Wilayani Kiteto Mkoani Manyara.

Awali akisoma mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi mahakamani hapo Mwendesha mashitaka wa Polisi Osca Kusara aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Michael Lepunyati ali,Richard Mlahagwa,Kipande Loguto Mgutyo, Lembrisi William, Daudi Willam, Meshaki Nyoroi Olotipwa, Zacharia Nyoroi Oletipwa

Wengine ni Mosonic Ngangwai, Loserian Isaya,Dijalo Kalapapai,Paulo Tunyoni Lemonyo (Kibaya )na Mohamed Said Kinyonga wa (Kibaya) ambapo kwa pamoja wamesomewa mashitaka tisa tofauti ya mauaji

Mwendesha mashtaka huyo wa Polisi alisema washitakiwa hao wanakabiliwa na kesi mbili tofauti ambapo shitaka la kwanza ni la jumla ya watu 3 waliuawa akiwemo Msagula Madole, Stivin Mashuhulu na mtu mmoa aliyejulikana kwa jina la Zungu

Na Shitaka la Pili ni la watu sita waliouawa akiwemo Saidi Hamad ,Emanuel Paulo (Mchungaji wa makanisa ya Pentekoste) mtoto wa Mchungaji aliyefahamika kwa jina la Shukuru Paulo (12) Mahaule Joseph, Zacharia Petro, na Rajabu Abdala

Ilielezwa Mahakama hapo kuwa watuhumiwa hao 12 kwa pamoja walitenda makosa hayo  tar 12 mwezi wa kwanza kuua kinyume na kifungu cha 196 sheria ya makosa ya jinai namba 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002

Hata hivyo watuhumiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kwakuwa Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji na kwamba kwa mujibu wa mwendesha mashitaka aliomba Hakimu wa Mahakama hiyo Nestory Barro kutaja tarehe nyingine ili kukamilisha ushahidi

Kwa mujibu wa Hakimu huyo mahakamani hapo alitaka tarehe nyingine ya kusikiliza kesi hiyo kuwa ni Feb 3 mwaka huu ambapo itawasilishwa tena na kwamba ushahidi utakapokamilika watyhumiwa hao watapelekwa Mahakama kuu kwa kesi hiyo kusikilizwa

Hata hivyo baada ya keshi hiyo kuahirishwa mahakamani hapo MTANZANIA ilizungumza na Shelunde Ngalula Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ambapo yeye alipongeza jitihada za Jeshi la Polisi kwa kuweza kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha mahakamani

“Ni kweli kwamba Polisi imefanya kazi yake ya kuwatafuta watu wanaodaiwa kuwa wauaji wa wenzao hivi karibuni Wilayani Kiteto na kusababisha vivo vya watu 10 na sisi cha kusimamia ni sheria ifuate mkondo wake”alisema Mwanasheria huyo

Alisema changamoto iliyopo ni ya kuwa ni jinsi gani ya kuwabaini wauaji kwani itatakiwa walioua wathibitishiwe bila shaka kuwa wametenda kosa hilo kwani hakuna anaebisha kuwa hakuna waliouawa na kuongeza kuwa sheria ifuate Mkoano wake

Hata hivyo miongoni mwa waliouawa ni pamoja na Mchungaji Emanuel Paulo wa makanisa ya Kipentekoste pamoja na mwanae Shukuru Paulo siku ya Juma Pili wakati wakienda kanisani hali iliyoibua hisia tofauti za watu

Pia miongoni mwa waliokamatwa ni pamoja na aliyekuwa Diwani wa kata ya Nameloko LeMichael Lepunyati (CCM) ambaye naye anatuhumiwa katika mauaji hayo wa watu 10 yaliyotokana na ghasia kati ya wakulima na wafugaji Wilayahi humo

Kwa Upande wake Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara Akili Mpwapwa  alisema kwa sasa juma ya watu 10 wako chini ya uangalizi wa pilisi,saba wameachiwa huru baada ya Polisi kujiridhisha kuwa hawana hatia na sita bado wanahojiwa

Wakati jitihada hizi zinaendelea baadhi ya wananchi Wilayani Kiteto wamethibitisha kuwa hali ni shwari kutokana na kufikishwa mahakamani watuhumiwa hao na kuongeza kuwa ili kukomesha vitendo hivi sheria ifuate mkondi wake bila kumwonea mtu

Mwisho

Maoni