POLISI KITETO WAKANUSHA UPORAJI WA SIMU


Polisi Kiteto wakanusha uporaji wa simu.

·         Waeleza wanaopora watu simu,pesa
·         Wasema mbali na uporaji pia watu wanapigwa

NA. MOHAMED HAMAD.
Jeshi la Polisi Wilayani Kiteto Mkoani Manyara limekanusha kuwa hakuna Askari aliyehusika kupora simu,pesa na baadhi ya mali za watu wanaotakiwa kuondoka  eneo la Emboley Murtangos kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari Nchini

Akizungumza hayo Foka Dinya Mkuu wa Polisi Wilayani Kiteto leo (jana) amesema siku waliyoporwa watu simu Polisi hawakwenda kwenye operesheni hiyo na waliokuwa wameenda ni Askari Migambo ambao huambatana nao kwenye Operesheni hiyo

“Tena aliyeandika habari hii nataka kumfahamu amepata wapi habari hizi,ninachojua siku hiyo pamoja na kwamba Polisi tunahusika kwenda kwenye  Operesheni hiyo  hatukuwepo siku hiyo Migambo ndio walienda”alisema Dinya

Wakieleza juu ya Operesheni hiyo mmoja wa maaskari ambaye jina lake limehifadhiwa alisema ktukana na sakata hilo walibaini mmoja wa Askari Migambo ambaye alihusika na kwamba ghatua za kinidhamu zinachukuliwa

Akizungumzia sakata hilo Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Umbulla alisema hana taarifa za watu hao kuporwa simu na mali zao na kuongeza kama kweli lipo tatizo la namna hiyo Jeshi la Polisi litashughulikia  

“Askari tumewapa masharti kuwa wasichukue kitu chochote cha mtuhumiwa hadi watakapowakabidhi Polisi na kama kuna aliyepora sheria kali dhidi yake zitafuata kwa kila atakaye husika”alisema Umbulla

Mkuu huyo wa Wilaya alieleza kuwa kuna mambo mawili yanayochanganywa na wananchi kuwa lipo agizo la Waziri Mkuu kutaka waliofanya mauaji ya watu kumi wakamatwe na pia kwa Wilaya tuna operesheni maalumu ya kuwatoa wavamizi katika eneo la Emboley Murtangos

Kwa mujibu Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Bruno Bongole ameliambia MTANZANIA kuwa jumla ya watu 99 wamekamatwa kwa tuhuma za kukutwa ndani ya eneo hilo huku 66 wakiwa wamefunguliwa mashitaka na 33 wakisubiri kuingizwa mahakamani kusomewa mashitaka yao

Baadhi ya wadadisi wa mambo wamesema kukamatwa kwa watu hao kumetokana na wengi wao kutojua mipaka ya eneo hilo utokana na madai kuwa kuna mkanganyiko wa mipaka uliofanya na Halamshauri baada ya kumalizika Kesi ta Msingi

Baadhi ya wananchi waliopo katika vijiji vinavyodaiwa kuunda hifadhi hiyo wamesema awali walikubaliana kutenga eneo hilo, baada ya kesi kumalizika eneo hilo limemega maeneo ya kilimo hivyo kusababisha malalamiko ambayo hadi sasa haijulikani mwafaka wake huku watu wakiendelea kukamatwa na kufikishwa mahakamani

Mwisho

Maoni