CCM KITETO WAMCHACHAMALIA MBUNGE WAO


CCM Kiteto wamchachamalia Mbunge
·          
                Wamtaka ajitokeze kukemea mauaji

NA.MOHAMED HAMAD
KATIBU wa Itikadi na uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilayani Kiteto Chrispipher Ole Parmet ameibuka na kumtaka Mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro kujitokeza na kukemea mauaji yanayoendelea kujitokeza Wilayani humo

Parmet amesema hayo siku ya wazazi kata ya Chapakazi alidai ukimya wa Mbunge Nangoro unawapa shaka wananchi na hasa wanachama wa chama chake  cha CCM ambao walitumia muda mwingi kumpata kiongozi hayo

"Tunataka mbunge wetu ajitokeze hadharani akemea maovu yanayoendelea hasa mauaji ambayo yanazidi kuwagawa wananchi kwa itikadi za ukabila na hata vyama hali inayosababisha wengi wao kukosa imani na Serikali yao”alisema Parmet

Migogoro ya ardhi Mkoani Manyara hasa Kiteto imekithiri kutokana na baadhi ya Viogozi kutokuwa waadilifu na kujali maslahi binafsi ambapo kwa muda mrefu imeendelea kurindika huku Viongozi wakionekana kutokuwa na dhamira ya dhati kumaliza

Kwa kipindi cha miezi minne zaidi ya wananchi 16 wamepoteza maisha huku zaidi ya 50 wakijeruhiwa kutokana na migogoro hiyo huku Viongozi wa Wilaya wakikwepa kuongea na wakulima na wafugaji kuwataka waachane na mgogoro huo

Parmeti amesema katika hali isiyokuwa ya kawaida Mbunge wao Benedict Nangoro (CCM) ameendelea kuwa kimya asijitokeze kukemea mauaji ayo hali inayotafsiriwa tofauti na kusababisha watu kuwa na chuki dhidi yake

“Chama tumemtaka Mwenyekiti kuonana na Mbunge ana kwa ana kuelezwa ajitokeze kwa wapiga kura wake na hata kwenda kuwapa pole wahanga wa mauaji hayo pamoja na kutoa msimamo wake kuhusiana na eneo hilo linalogombaniwa”

Alisema Migogoro ya ardhi Wilayani Kiteto inasababishwa na baadhi ya viongozi Wilayani humo ambao wana maslahi na eneo la Emboley Murtangos kutaka kutimiza matakwa ya jamii moja ya kifugaji ili waweze kunufaika na eneo hilo

Akifafanua zaidi Katibu huyo amesema eneo la Emboley Murtangos lina utata mkubwa ambalo hata Waziri Mkuu wa Mizengo Pinda baada ya mauaji aliagiza kutazamwa upya juu ya eneo hilo ambalo linaonekana kuwepo kwa utata wa uanzishwaji wake

Alisema baada ya kutembelea eneo hilo alichokiona sio hifadhi kama inavyodaiwa na Viongozi wa Wilaya bali alikuwa mashamba ya wakulima na kusisitiza viongozi wa Halmashauri  kuangalia lengo la uanzishwaji wa hifadhi hiyo upya pamoja na mipaka yake

Pia Waziri Mkuu alishangazwa kusikia jamii ya kifugaji wamasai wamechangishwa fedha za kuwatoa wakulima katika eneo hilo la Emboley Murtangos hali aliyodaiwa kuleta uvunjifu wa amani na kusababisha kikundi cha watu kuibuka na kufanya mauaji katika maeneo hayo

Mwisho

Maoni