DC KITETO AKIRI WAFUGAJI KUWA TISHIO LA WAKULIMA


DC Kiteto mipaka ni tatizo la mauaji ya wakulima,wafugaji

NA. MOHAMED HAMAD
Mauaji yanayoendelea kujitokeza Wilayani Kiteto Mkoani Manyara kati ya walikuma na wafugaji inasababishwa na kutobainishwa kwa mipaka kwa muda mrefu hivyo kila mtu kufanya atakavyo

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Jaki Umbulla kwenye mkutano mkuu wa Kijiji cha Kimana uliohudhuriwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama pamoja na baadhi ya viongozi waandamizi wa Mkoa wa manyara

“Tatizo tulilonalo hapa ni wananchi kushindwa kutambua wako eneo gani katika kufanya shughuli zao za kilimo ama ufugaji kwani awali tulitenga maeneo hayo kwa utaratibu maalimu na baadae ukavurugika”alisema Umbulla

Kinachoniudhi sana ni kuona idadi kubwa ya watu kutoka maeneo ya jirani kuja kuhodhi maeneo makubwa ya adhi huku Kiteto kwa shuhuli za kilimo huku wanaKiteto wakiwa hawana hata hatua moja ya kulima

Amesema utaratibu huu haukubaliki na hata kama walipewa na Serikali za vijiji kwa kuhonga kwao haikubaliki lazima wanyan’ganywe tuanze upya utaratibu huu wa kugawa ardhi kulingana na idadi ya wananchi wetu tulionao

“Unamkuta mtu ana zaidi ya ekari elfu 3 huko porini na hata kuingilika inakuwa shida huu sio utaratibu wa matumizi bora ya ardhi na hata hiyo Halamshauri haiwezi kunufaika na chochote humo kwani hata usalama wenyewe kufika ni mdogo”

Kuhusu eneo hilo kuitwa hifadhi ya Emboley Murtangos Umbulla alisema vijiji saba vilikwisha tenga eneo miaka ya 2000 kwa makubalian maalumu na vikao vya kisheria pamoja na kumbwa kuna wajanja wachache waliiba mihutasari bado tunatambua eneo hilo
Kauli hiyo iliibia hoja nyingi kwa wananchi hao wakisema kamwe hawakubalinani na jina hilo la Emboley Murtangoso bali wanatambua kutenga hifadhi kwakuwa wanachofahamu kila kijiji kilitenga eneo lake la matumizi ya baadaye na sio kama inavyoelezwa

“Tusipotoshane hapa baada ya kuharibika jambo hili, ninachokubuka mimi ni mwanzilishi wa mipango hii mwaka 2000 tulikuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi ambapo hapo tulisema tuwe na sehemu ya akiba kidogo kwa watu watakao ongezeka wapatiwa”alisema Bakari Maunganya

Alisema wakati wanatenga hakukuwa na kitu kinachoitwa Emboley Murtangos kama eneo linavyolazimishwa kutambulika kisheria kwa nguvu ya wachache ya upande mmoja (wafugaji) kulitumia kwa makazi yao pamoja na kulisha mifugo …(makofi)

Kwa upande wake Wilson Ngolanya (mkulima wa kimana) alisema baada ya kutenga eneo hilo jamii ya kifugaji (wamasai) walionekana kuhodhi eneo hilo kwa shughuli zao hali iliyosababisha wakulima nao kuingia na kuanza shughuli za kilimo

Katika mvutano huo Ngolanya alisema hapo ndipo chanzo cha mauaji yakaanza kwa jamii ya baadhi ya kifugaji kuwa na mamlaka ya kuanza kufanya watakavyo kama kuvamia wakulima na kuwaua huku Serikali ikiendelea kuwaunga mkono kwa kuwakamata wakulima na kuwafunga

Nae Anon Chui (mkulima) alisema adui namba moja wa matatizo hayo ni Serikali yao kuanzia ngazi ya kijiji,kata,Wilaya na hata Taifa hasa pale ilipoungana na wafugaji kuwachangisha fedha kisha kuwaondoa wakulima katika maeneo hayo

Amesema kama wakulima na wafugaji wanakamatwa kwa kuitwa wachochezi na kufikishwa mahakamani  hali kadhalika viongozi hao nao wanatakiwa kukamatwa kwa kuanzisha mipango mibovu na kuiunga mkono

Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya alisema Serikali imejipanga kuainisha mipaka ili kila kundi liweze kutambua eneo lake wakati wanafanya shughuli zao za kujipatia kipato akisisitiza kuwa eneo hilo lilitengwa na vijiji saba na mahakama ikaamuru pasiwepo na shuguli za ibinadamu huko

Mwisho







Maoni