MADIWANI KITETO WAHOJIWA KUHUSU HIFADHI YA MURTANGOS


Madiwani 13 Kiteto kuhojiwa kuhusu Hifadhi ya Emboley

NA.MOHAMED HAMAD
JUMLA ya madiwani 13 wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara wanatarajia kukutana na tume maalumu ya makamishna waliopo Mkoani Manyara juu ya sakata la migogoro ya ardhi Wilayani humo inayoendelea kusababisha maafa

Madiwani hao wamepata Barua kutoka ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Kiteto kwa njia ya dispachi kwa lengo la kuonyesha umuhimu ambao unakusudiwa kuleta matunda ya kuunganisha wakulima na wafugaji waliopoteza mahasimiana na na kusababisha mauaji ya mara kwa mara

“Napata shaka sana kwenda kuhojiwa na makamishna hao sijajua nini wanataka kwangu hasa kuhusiana na migogoro ya ardhi kwani mbona kila kitu kinajulikana na awali walichukua vielelezo vingi tu na nyaraka?”alisema Diwani mmoja Wilayani humo

Alisema Serikali ikitaka kukomesha mauaji Kiteto inaweza lakini kama itaingiza siasa kwa kulindana hasa uchama,ukabila,urafiki watu watazidi kupoteza maisha huku wengi wao wakiwa maskini kukatishwa maisha yao bila sababu

Kidawa Othmani Kidawa Diwani wa Kata ya Matui ni miongoni mwa madiwani waliopata barua ya wito rasmi ambapo pamoja na mambo mengine amesema jambo hili ni zito linahitahi umahiri na umakini katika kulishuhulikia kitokana na kushamiri siasa, ukabila na rushwa

Uchunguzi uliofanywa na MTANZANIA umebaini kuwa zaidi ya makundi manee yanaendelea kuhojiwa kutokana na sakata la migogoro ya ardhi Kiteto wakiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Jaki Umbulal,aliyekuwa Mkurugenzi Jane Mutagurwa ambaye sasa amehama

Wengine ni Mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedicti Ole Nangoro,Mwenyekiti wa Halmashauri Mainge Lemalali,Afisa habari wa Halmashauri Maiko William,pamoja na maafisaa wengine ambao majina yao hayajafahamika mapema

Mbali na viongozi hao pia kada ya wanasiasa (madiwani) 13 wamepatiwa barua rasmi kwaajili ya kwenda kuhojiwa kuhusu sakata hilo ambalo linazidi kuchukuwa sura mpya kila kukicha kwa wakulima kupoteza maisha pamoja na majerhi mara kwa mara na kundi la wafugaji

Hata hivyo habari za uhakika zinaeleza kuwa wenyeviti wa vijiji saba pamoja na watendaji wao katika vijiji saba vilivyounda eneo hilo la hifadhi ya Emboley nao wanaendelea kuhojiwa kuhusu uhalali wa hifadhi hiyo na kama ilifuata taratibu za uanzishwaji

Wakati mahojiano haya yakiendelea jamii ya kifugaji wamasai wamezidi kuwajeruhi wakulima wakiwa mashambani pamoja na kulisha mifugo yao hali iliyodaiwa kuwa inazidi kuleta chuki uhasama pamoja na wananchi kukosa imani na Serikali yao

Mwisho

Maoni