Kinana awashukia viongozi wa Serikali
  • ·         Asema wanachangia migogoro ya ardhi
  • ·         Aapa kuwasilisha kilio cha wananchi kwa Rais
  • ·         Akiri migogoro yaanzia kwenye CCM

NA.MOHAMED HAMAD
KATIBU Mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Taifa Abrahamani Kinana amewashukia viongozi wa Serikali kushindwa kuwahudumia wananchi hali inayo sababisha wakose imani na Serikali yao

Akizungumza kwenye ziara yake Wilayani Mkoani Manyara Kinana amesema kila kona ya nchi kuna migogoro ya ardhi na kuahidi kilio hicho kuwasilifikisha kwa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete ili aweze kutafutia ufumbuzi

Alisema migogoro ya adhi imekuwa tishio kwa wananchi kuuwana wenyewe kwa kusababishiwa na baadhi ya viongozi wasiokuwa waadilifu ambao wamekuwa wakiitumia migogoro hiyo kama vyanzo vya mapato yao

“Migogoro hii inaanzia ndani ya chama changu cha CCM, siamini kama kuna jitihada za vongozi wa Serikali zilizofanyika kutatua migogoro naahidi suala hili nitaenda kumweleza Mhe Rais ili aweze kuishuhulikia”

Wakati mwingine viongozi hatuonyeshi dhamira ya dhati kushuhulikia matatizo,tunaenda kwa wananchi usikiliza migogoro na kurejea tukiwa hatujaishihulikia,lakizima madhara yajitokeze alisema Kinana huku wananchi wakipiga makofi mengi

Alisema suala hili mwenye uwezo kulishuhulikia ni Mhe Rai Peke yake na ndio maana hakutaka kusikiliza kauli za wananchi kwenye  baada ya kusomewa taarifa nyingi za chama na hata Serikali

Kuhusu suala la katiba mpya,Katibu mkuu huyo wa CCM alisema wananchi wa Tanzania hawaihitaji bali hilo ni shinikizo la baadhi ya viongozi wakitaka kuingia madarakan kwa kushinikiza umma kutaka katiba

“Wananchi wanahitaji huduma za jamii kama vile maji, afya, barabara na shule na sio katiba kwani ziko nchi zinazoongozwa bila katiba mfano Uingereza mbona wananchi wanaishi kama haja ni kuwa na katiba”alihoji Kinana

Baadhi ya wananchi wa Kibaya katika mkutano huo walikosoa hutuba hiyo wakisema walichotarajia ni kusikia hatua zaidi kuhusu migogoro ya ardhi ambayo imesababisha zaidi ya watu 16 kufunguliwa kesi za mauaji huku 77 wakifungwa na wengine zaidi ya kumi kupoteza maisha kwa kuuawa

“Nilitegemea Kinana asema viongozi waliohusika kusababisha vurugu hizo wamechukuliwa hatua hii,na sio kuja na kusema naenda kwa Rais, hiyo haitoshi kwani Rais anajua kila kitu tunataka kuona hatua zikichukuliwa”alisema Mashaka Saidi Fundi mwananchi wa Kibaya

Mwisho



Maoni