MIGOGORO YA ARDHI NANI WAKULAUMIWA KITETO



MAKALA YA ARDHI KITETO -1

Migororo ya ardhi nani alaumiwe Kiteto?
Na.Mohamed Hamad Kiteto.
Kwa mujibu wa vitabu vitakatifu ambavyo vinatumiwa na makundi mbalimbali ya kijamii vimeeleza kuwa asiyefanya kazi na asile,kauli hii imewasukuma waliowengi kufanya kazi ili waweze kutafsirika vizuri ndani ya jamii na nchi yao kwa ujumla.

Msimu wa masika na kiangazi hapa nchini na hasa wilayani Kiteto mkoani Manyara umekuwa taabu na mateso kwa jamii za wakulima na wafugaji kwakuwa wamechagua kuendesha maisha yao kwa kufanya shughuli hiyo ama zote kwa pamoja.

Kutokana na maamuzi hayo kazi hizo zimegekuwa shubili kwa pande hizo badala ya neema baada ya kuanza kuuana kwa kilichodaiwa kugombea ardhi kwaajili ya shuhuli za kuliletea maendeleo kilimo na ufugaji

“Baba wa Taifa enzi za uhai wake aliweza kuwakamata wasiofanya kazi na kuwafungulia mashitaka akiwaita wazururaji hali ambayo wengi wao walishika adabu na kuanza kufanya kazi ya kujipatia  kipato”

“Mimi ni miongoni waliokubwa na sakata hili la kukamatwa kwa miaka ya nyuma enzi za ujamaa, tulikamatwa na wenzangu kisha kufunguliwa mashitaka wengi wetu tulikutwa mijini tukitakiwa kurudi vijijini tukalime ama kufuga”alisema Maulidi kijongo (mkulima)

Hali hii ilitulazimu hata tulipotaka kwenda kuhitaji bidhaa mijini tuwe makini ili tusikamatwe na kuitwa wazururaji ikijengwa hoja ya kila mtu lazima afanye kazi ya kumwingizia kipato chake ama familia yake

Ni kutokana na msingi huo leo utawaona watu wakilazimika kufanya kazi ingawa ule utaratibu wa kukamatwa tena kwa madai ya uzurura mijini haupo lakini kuna changamoto kibao zinazotokana na kufanya kazi

Mkulima huyo alitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na uzalishaji wa mazao hayo kwa shida aidha iwe ya mifugo ama kilimo kutokana  na sababu mbalimbali zikiwemo za kusababishiwa ama za kimazingira

Akizungumza bila kumumunya maneno mkulima huyo ataja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni migogoro ya ardhi ambayo imekuwa tishio kwa maisha ya wananchi ambayo imedaiwa kusababishwa na baadhi ya viongozi wasio kuwa waadilifu

Migogoro hiyo imeelezwa kuwa imetokana na makundi hayo ndani ya jamii kugombanishwa kwa maksudi na baadhi ya watawala wasio kuwa waadilifu wakinufaika na ugomvi huo ambao mwisho wa siku watu wanapoteza maisha

Uchunguzi uliofanywa na makala hii umebaini kuwa kuna baadhi ya viongozi wa ngazi za vitongoji,vijiji, kata,na hata Wilaya wamekuwa na mamlaka ya kuuza ardhi kwa wanaohitaji huku wakijua  eneo hilo sio mahsusi kwa kazi husika

Pamoja na kubainika kwa watawala hao hakuna hatua iliyowahi kuchukuliwa dhidi ya viongozi hao na watawala wa ngazi ya Wilaya na hata mkoa jambo ambalo limedaiwa kuzoeleka na hakuna wa kumdhibiti mwnzake

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Jaki Umbulla ni miongoni mwa viongozi walioweza kuzungumza hadharani kuwa kuna baadhi ya viongozi wasio waadilifu tena akiwa na taarifa za uhakika kuhusu viongozi hao

“Kuna baadhi ya viongozi wenzetu wasio waadilifu ndani ya jamii  wamekuwa tatizo kubwa katika migogoro ya ardhi na hili nawataka wajirekebishe mara moja kwani madhara makubwa yanazidi kujitokeza”alisema Umbulla

Wakati mwingine unakuta mtu anauziwa ardhi na kiongozi kufanya kazi ya kilimo wakati eneo hilo ni la mifugo ama kufanya kazi ya mifugo wakati eneo hilo ni kilimo hali hiyo imefahamika na hakuna hatua zinazochukuliwa”alisema Bakari maunganya (mkulima)

Alisema malalamiko hayo yamewasilishwa kila kona ya wilaya mkoa na hata Taifa cha ajabu hakuna hatua iliyowahi kuchukuliwa ya kuwaadhibu viongozi na hata wananchi waliohusika kukiuka sheria hizo

“Wakati mwingine mtu unasema labda nimekuwa kero ndani ya Ofisi za Serikali kwani kila mara lazima kuripoti kueleza matatizo yetu, chaajabu hatuoni hatua zozote ni kulindana tu kwa Serikali hii inaumiza sana”alisema kwa hisia kali

Kila mara wakulima na wafugaji Wilayani Kiteto wamekuwa wakipoteza maisha ambapo mapema mwaka huu mwezi wa pili mwaka huu zaidi ya watu kumi waliuawa kinyama huku kila baada ya muda wengine kadha nao hupoteza maisha na hivi karibuni Aug 7 zaidi ya watu watano waliuawa

ITAENDELEA WIKI IJAYO…..




Maoni