MABADILIKO YA TABIA YA NCHI YAATHIRI KITETO



Mabadiliko tabia ya nchi yaathiri wananchi Kiteto

Na.Mohamed hamad Manyara
MABADILIKO ya tabia ya nchi yanayotokana na sababu mbalimbali nchini zikiwemo uharibifu wa mazingira yameanza kuleta madhara kwa wananchi wilayani kiteto mkoani Manyara yakiwemo uhaba wa maji, pamoja na kuibuka kwa magonjwa ya binadamu na mifugo

Wakizungumza kwenye mafunzo ya siku moja wadau wa mabadilko ya tabia ya nchi yaliyoandaliwa na shirika la Msalaba Mwekundu Kiteto walisema madhara makubwa yanayoendelea kujitokeza na kuwataka wananchi kuwa tayari kukabiliana na janga hilo

Mratibu wa shirika la msalaba mwekundu wilayani Kiteto Miraji Salmu  alisema madhara yanazidi kujitokeza kutokeza kutokana na kukosekana taarifa sahihi za hali ya hewa pamoja na elimu duni ya namna ya kufikia taarifa hizo

“Madhara ya mabadiliko ya tabia ya nchi yanazidi kujitokeza ambapo Kiteto ni moja kati ya wilaya mbili Tanzania zilizoteuliwa kukabiliana na janga hili ambapo kwa Afrika nchi ya Tanzania na Malawi ndio zilizopendekezwa kukabiliana na janga hilo”alisema Miraji

Akieleza mipango na mikakati ya kukabiliana na janga hilo mkurugenzi mtendaji wa shirika la msalaba mwekundu Tanzania Renatus Mkaruka alisema shirika lake limeamua kuunganisha nguvu ya pamoja na mashirika mengine ulimwenguni kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi

Alisema watafanya kazi kwa kushirikiana na mashirika mengine katika kukabiliana na janga hilo yakiwemo shirika la Afya Duniani  (WHO),mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA), shirika la chakula duniani (WFP) na UDSM ambayo kwa pamoja yatafanya kazi tofauti

Bw.Mkaruka ametaja maeneo yatakayo shughulikiwa kuwa ni pamoja na umoja na  kuangalia usalama wa chakula, lishe, afya, pamoja na namna ya kupunguza athari za maafa ndani ya jamii

Akieleza historia ya mradi huo Mecklina Merchades kutoka mamlaka ya hewa Tanzania (TMA) alisema mchakato wa kukabiliana na janga hilo ulianza mwaka 2009 huko Geniva ya uswisi ambapo nchi kadhaa zilikutana kujadili namna ya kukabiliana na janga hilo

“Watafiti wamegundua kuwa majanga yataendelea kujitokeza hivyo mradi huu utasaidia kuwapa elimu wananchi ya jinsi ya kukabiliana na majanga hayo ambayo madhara yake ni kupoteza maisha ya viumbe hai wakiwemo wanadamu na hata mifugo”alisema

Alitaja baadhi ya maengo ya mradi huo kuwa ni pamoja na kupunguza athari zinazotokana na mabadiliko ya tabia ya nchi, kufanikisha kutekelezwa kwa malengo ya nchi, taarifa kutumika katika mipango ya utekelezaji,pamoja na kuboresha miundombinu iliyopo

Kwa upande wake Amani Abrahamu (mfugaji) alisema madhara yanayoendelea kujitokeza katika maeneo ya Makami wilayani Kiteto ni pamoja magongwa ya mifugo kuendelea kuibuka, na ya binadamu hali inayotishia kizazi cha jamii ya kifugaji kutoweka

“Sisi wafugaji wa jamii ya kimasai hatuna utamaduni wa kuweka fedha benki na ndio maana tunawekeza kwenye mifugo tukielezwa kupunguza mifugo kutokana na janga hili ni sahihi ila elimu zaidi inatakiwa kutolewa kwani hakuna mfugaji anayeridhia kwa hivi sasa

Zaidi ya washiriki 20 kutoka mashirika ya umma yanayofanya kazi zinazofanana katika kukabiliana na tabia ya nchi likiwemo shirika la KINNAPA,NAADUTARO,na watendaji wa vijiji vinavyotekeleza mradi huo vya Orpopong’i, Ndaleta, makami, na Ndedo wameshiriki katika warsha hiyo ya siku moja mjini Kibaya

Mwisho

Maoni