MIGOGORO YA ARDHI IKOMESHWE KITETO -4


Picha za mauaji yaliyofanyika Dec 2012 Kiteto kati ya wakulima na wafugaji wakigombea ardhi hapa wako katika chumba cha maiti Hosp ya wilaya ya Kiteto Manyara Picha na Mohamed Hamad Kiteto



Migogoro ya ardhi Kiteto ikomeshwe-4

Na.Mohamed  Hamad Kiteto
MAKALA iliyopita iliishia sehemu inayosema kuwa, kama Rais atakuwa ameamua kumtuma kwa mara  nyingine Waziri Pinda basi aje kuonana na wananchi wenyewe ambao ni wakulima na wafugaji kila mmoja aseme nani alihusika na kwa kiwango gani kuchangia mgogoro huo na sio kuongea na waliosababisha wa mgogoro peke yao.

Wiki hii makala inaangazia hatua ya mgogoro wa ardhi Kiteto mkoani Manyara kutinga Bungeni kutaka msaada zaidi ili kunusuru maisha ya wakulima na wafugaji wanaoendelea kuhasimiana kila kukicha yalindwe baada ya kuonekana kuwa hatarini

Wakati mwingine wakulima na wafugaji wilayani Kiteto wamedai kuwa wanaisha maisha ya wasiwasi wanapofanya shughuli zao za kujitaftia riziki kutokana na uhasama uliojengeka kati yao

Malalamiko hayo yamewasilishwa kwa viongozi mbalimbali wa chama na Serikali katika ngazi tofauti hapa nchini kunusuri, lakini bado hali inazidi kuwa tishio na wakati mwingine wananchi hao wamedai kuwa sasa wameamua kumwachia Mungu

Wakati kauli hiyo ikionekana kuwa ni ya kukata tamaa dhidi ya viongozi wao ambao wamedai wameshindwa kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo unaosababisha mauaji ya mara kwa mara mgogoro huu umetinga Bungeni

Katika kuwahakikishia Watanzania kuwa suala hili Serikali imeamua kulivalia njuga Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Manyara na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Jaki Umbula aliibukia Bungeni na kusema Waziri Pinda ameshakabidhiwa kazi hiyo

Alisema suala hili linashuhulikiwa kwa undani kwani baada ya tatizo hili kuonekana kwa viongozi wa ngazi za juu akiwmo Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Dodoma alisema suala hili litashuhulikiwa na Waziri Mkuu Pinda

Alisema pamoja na mambo mengine alichojifunza akiwa Bunge la Katiba ni pamoja na  maridhiano kwa viongozi wanapowaongoza wananchi na pasiwepo na tabia za kujitaftia umaarufu majukwaani

Akichangia taarifa kamati za Bungeni la katiba Martha Jaki Umbulla alisema “mgogoro wa ardhi unahitaji maridhiano ya viongozi na si kwenda majukwaani inachochea uhasamakati ya viongozi na hata wananchi wenyewe”

“Nimejifunza kitu kizuri sana, maridhiano ni nmuhimu badala ya viongozi kwenda kwenye majukwaa ya kisiasa na kuzungumzia migogoro na kuzidi kupanua wigo wa mitafaruku ni vizuri tukarudi kwenye maridhiano”

“Sitaki kuingia kwa undani sana kwasababu Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania analishuhulikia kwa ukaribu na hata Rais wetu akiwa katika ziara yake Dodoma aliliona na kusema litashuhulikia kwa umakini zaidi”alisema Umbula

Hata hivyo kauli hiyo imetokana na lalamikola la Mbunge wa Kongwa Job Ndugai kuwa Rais Jakaya Kikwete akiwa ziarani Kongwa alilalamikiwa juu ya mauaji yanayoendelea kujitokeza kila mara wilayani hapo

“Mheshimiwa Rais, kule Kiteto ni majirani zetu kuna mauaji ya kutisha kila mara napokea maiti za watu wangu waliouawa huko mashambani kuna uongozi lakini uko kimya na hawajawahi hata siku moja kushiriki mazishi hali hii inasononesha sana naomba kauli ya Serikali”alisema Ndugai

Wakulima kutoka maeneo ya Kongwa wanauawa na kuambiwa kuwa ni wavamizi Serikali ina mpango gani kuwasaidia watanzania hawa wasio na hatia?huu ubaguzi ni mpaka lini mbona Baba wa Taifa alikemea”alisema Ndugai huku akionyesha kukerwa na kitendo hicho cha mauaji

Hata hivyo kuwasilishwa kwa taarifa hiyo Bungeni na Mb. Viti maalumu mkoa wa Manyara Martha Umbulla kumetafsiriwa kuwa ni kujibu shambulizi dhidi ya Mbunge wa Kongwa Job Ndugai na Chemba Juma Nkamia kuhusu kuendelea kuutuhumu uongozi wa Kiteto kushindwa kuzuia mauaji ya watu wasiokuwa na hatia

Waharakati wa haki za Binadamu wameelezea hali inayoendelea kujitokeza Kiteto ni  kukwepa majukumu kwa viongozi hao na kwenda kuongelea suala hili Bungeni kwani awali walipaswa kudhibiti mauaji kabla ya kujitokeza

Mashaka Saidi Fundi mwangalizi wa haki za binadamu Wilayani humo alisema mgogoro wa ardhi Kiteto umedumu kwa miaka mingi huku kukiwa hakuna dhamira ya dhati kutatua huku sheria zikiendelea kukiukwa na viongozi

Alisema chanzo cha mgogoro huo ni mkanganyiko wa kuanzishwa hifadhi ya jamii ya Emboley Murtangos ambayo ilidaiwa kuwa chini ya vijiji saba vilivyoizunguka kuwa hakukuwa na dhana shirikishi bali kulikuwa na ujanjaujanja

“Hakuna Kiongozi mkweli anayezungumzia mchakato wa kuanzisha hifadhi hiyo kuwa itamnufaisha nani kwani hata baadhi ya vijiji  vilivyodaiwa kutenga eneo hilo vinalalamika kuwa hawakushiriki  kikamilifu”alisema Fundi

Alisema malalamiko haya yanatia shaka kubwa kisheria ambapo kwa hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Jaki Umbula akiongea na vyombo vya habari alisema  hata mihutasari yenyewe ya vijiji vilivyounda hifadhi ya Emboley Murtangos baadhi ilibwa

Akiongea kwa kujiamini Fundi alisema suala hili ana nia ya kuifikisha Halmashauri mahakamani kwa kutumia mamilioni ya fedha kwaajili ya zoezi hilo ambalo hata watunga sera wenywe madiwani  wamekuwa wakitofautiana katika kulishuhulikia

“Nitakwenda mahakamani kuishitaki Halmashauri kwa kujiingiza kwenye mgogoro wa vijiji ambao hauko rasmi kwani inaonekana suala hilo kama linashuhulikiwa kimila na kiukabila zaidi”alisema Fundi na kuongeza

Tulishuhudia wafufaji wakilalamika mbele ya Waziri Mkuu Pinda kuchangishwa mamilioni ya fedha kwaajili ya kuendesha kesi dhidi ya wakulima jambo hili lina utata mkubwa linahitaji ufumbuzi wa kisheria”alisisitiza

Alisema hata kama mihtasari imeibwa Serikali ya Kiteto itahakikisha kuwa inapatikana kwani nia na dhamira ya kuanzishwa hifadhi ipo na watu wapo hivyo hauwezi kukwamishwa na watu wachache wasio kuwa na nia njema alisema Umbulla

Pamoja na suala hili kutinga bungeni na kuzungumzwa kama tatizo bado Waziri Mkuu ametwishwa zigo hili kutafuta ufumbuzi watu wasiendelee kuuana na nnjia pekee ya kutumia ni kutafutwa uhalali ya kuanzishwa hifadhi hiyo na manufaa yake


masarade1995@gmail.com 0787 055 080








Maoni