MIGOGORO YA ARDHI KITETO NANI ALAUMIWE -2



 Waziri Mkuu Pinda akiwa ziarani Kiteto kuhusu migogoro ya ardhi

Migororo ya ardhi Kiteto nani alaumiwe?

Na.Mohamed Hamad Kiteto.
MAKALA ya wiki iliyopita iliishia sehemu inayosema kuwa  Kila mara wakulima na wafugaji Wilayani Kiteto wamekuwa wakipoteza maisha ambapo mapema mwaka huu mwezi wa pili  zaidi ya watu kumi waliuawa  huku kila baada ya muda wengine kadhaa hupoteza maisha…

Kutokana na mgogoro huu makundi mabalimbali ya kijamii wasomi na hata watu wa kawaida kabisa wameweza kuzungumzia sakata hili ambapo makala hii imeamua kuwapa nafasi ili uweze kujua mgogoro wa ardhi  Kiteto nani alaumiwe?

Awali miaka ya 1992 Shirika la (LAMP) Land Manegement Programme lililokuwa chini ya SIDA kutoka Sweden liliwezesha zaidi ya vijiji 35 wilayani kiteto kupanga matumizi bora ya adhi ili kuondoa mgogoro wa wakulima na wafugaji

Kwa mujibu wa Viongozi wa shirika hilo na pia uongozi wa Wilaya ya Kiteto walikiri kutumia mamilion ya fedha katika mipango hiyo ili kuondoa mgogoro kati ya makundi hayo

Kadiri siki zilivyozidi kuongezeka watu na mifugo iliongezeka na migogoro iilijitokeza huku kukiwa na mamlaka za ukabiliana na tatizo hilo na wasiweze kuzua migogoro hadi hatua ya mauaji ilipoweza kujitokeza

Kwa mujibu wa kauli za viongozi Wilayani Kiteto wamekuwa wakisema chanzo cha migogoro hiyo  ni watu kutoka nje ya Wilaya ya Kiteto kuvamia maeneo kwa kufanya shughuli za kilimo

Mainge Lemalali Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto alikaririwa katika moja ya vikao vya Halmashauri  akisema watu wa Wilaya ya Kongwa wamekuwa tatizo Kiteto kuvamia maeneo yao na kufanya shuhuli za kilimo

“Kwa sasa hatuhitaji kuona Kiteto inageuka kuwa jangwa kama ilivyo maeneo mengine na hapa nchini nasisitiza kuwa yoyote atakaye ingia bila taarifa na kufanya shuhuli za kilimo huko maeneo tuliyokataza sheria itafuata mkondo wake”alisema Lemalali

Mbali na kauli hiyo pia Lemalali alitoa wito kwa Serikali ngazi ya Taifa kuingilia kati mgogoro huu ambao hata wao wamedai umewashinda kwani waliopo katika maeneo hayo ni baadhi ya vigogo ambao wamejichimbia mizizi katika mapori yaliyohifadhiwa ya Emboley Murtangos

“Tumetumia gharama kubwa sana kuwaondoa wakulima waliopo katika maeneo tuliyotenga na hapa naweza kusema kuwa ni zaidi ya mamilioni ya fedha yaliyotumika lakini bado watu hawatoki na wanaendelea na uharibu  mazingira uongozi wa juu uingilie kati”alisema Lemalali

Mbali na kauli hiyo pia alimtaka Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jobu Ndugai kuwakataza wananchi wake ambao wamevamia maeneo ya kiteto na wameapa kutotoka kwa madai wako kihalali

“Nimtake tu Kiongozi wetu Ndugai atumie fursa aliyonayo kuongea na wananchi wake wasivamie maeneo ya Kiteto na kufanya shuhuli za kilimo ambazo zimekuwa na madhara kuharibu mazingira Kiteto hatutaki kuharibiwa maeneo yetu na wavamizi”alisisitiza Mainge

Kwa upande wake Job Ndugai akiongea kwa njia ya simu juu ya wananchi wake kudaiwa kuvamia eneo la kiteto na kufanya uharibifu wa mazingira alisema anasikitishwa na kauli za kibaguzi zinazotolewa na viongozi wa Kiteto kuwaita Watanzania wenzao kuwa ni wavamizi

Sidhani kama tumefikia hatua ya kuitana wavamizi ndani ya nchi yetu, Baba wa Tifa Mwalimu Julius Nyerere alikemea sana vitendo vya ubaguzi kwa itikadi za kidini kikabila na hata rangi na kwamba amewataka wananchi wawapime viongozi hao

“Wananchi muwapime viongozi wenye sura za ubaguzi na niwaombe kila Mtanzania ana haki ya kuishi mahali popote ilimradi asivunje sheria sasa kama kuna aliyevunja sheria tena kwa kufanya kazi sio kuiba ama kufanya uhaini  hapaswi kuuawa  bali sheria ifuate mkondo wake

Alisema kila mara mauaji yamezidi kujitokeza Kiteto na wanaouawa ni watanzania wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma jirani na wilaya Kiteto hivi nani anayewaua Watanzania hawa na huko Kiteto hakuna viongozi wa kushuhulikia matatizo haya

Naiomba Serikali ngazi ya juu iweze kuingilia kati kuokoa watu hawa ambao wanauawa bila hatia na kikundi cha watu wachache wanaojiita walinda mazingira na ambao hawajakamatwa mpaka leo… alisema ndugai kisha simu yake kukatika

Kutokana na mgogoro huu viongozi mbalimbali wa ngazi ya Mkoa na Taifa wa chama na Serikali walifika Kiteto kushuhudia mauaji hayo na pia wengine walifika kutaka kujua kilichopo hali iliyotafsiriwa kuwa kazi hiyo bado ni ngumu

Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni miongoni mwa viongozi wakuu ngazi ya juu Serikalini aliofika Kiteto na kuahidi kuwa suala hili ataenda kuongea na Mhe Rais Kikwete toka mwezi wa pili mwaka huu
Na hata hivyo baada ya kuondoka mauaji yaliendelea ambapo zaidi ya watu nane waliuawa kikatili kukatwakatwa mapanga na wengine kuchinjwa wakigombea ardhi

Hali kadhalika Katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Abrahamani Kinana alifika Wilayani humo kuongea na wananchi ambapo alisema kuna matatizo lukuki na ambayo kwa nafasi yake atahakikisha kuwa anakaa na Rais Kikwete kumweleza alichokiona

Hata hivyo Rais Kikwete katika ziara yake mkoani Dodoma alilalamikiwa na wananchi kuwa kila mara wameendelea kupokea maiti za ndugu zao wanaouawa katika maeneo ya kiteto hivyo wamechoka na kumtaka Rais atoe tamko

MAKALA ITAENDELEA WIKI IJAYO…

Maoni