CELG:Manyara yaongoza kwa ukatili 71%

CELG:Manyara yaongoza kwa ukatili 71%
·         
           Wanafunzi Sekondari Babati walaani ukatili huo

NA.MOHAMED HAMAD MANYARA.
Tafiti zilizofanywa na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali hapa nchini ikiwemo Wizara ya Afya mwaka 2013 imebainika kuwa mkoa wa Manyara unaongoza kwa vitendo vya ukatili kwa 71% dhini ya mikoa mingine

Wizaya ya Afya ilifanya utafiti mwaka 2013 kuwa mkoa wa Manyara unaongoza kwa ukatili wa ukeketaji kwa 71%,Dodoma kwa 64%, Arusha 59%,Mara 40,Morogoro 21, na Tanga 20% ambapo CELG imeamua kuingilia kati ili kuutokomeza

Kituo cha utawala wa sheria na mazingira (CELG) chini ya ufadhili wa LSF kutokana na tafiti hizo kimeweka kambi katika wilaya za Kiteto,Babati,Mbulu na Hanang mkoani Manyara ili kukabiliana na ukatili huo ambao umedaiwa kuwa tishio kwa jamii hizo

Awali akielezea malengo ya kituo hicho jana mbele ya wanafunzi kutoka shule za Sekondari Kwaraa,Babati day  na Eloni Sekondari mwezeshaji toka kituo cha CELG Emmanuel Mgalla alisema madhara ya ukatili yamezidi kujitokeza kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za wananchi kukata tama na kuendekeza ukatili huo

Alitaja aina za ukatili huo kuwa ni ukatili wa  Kiuchumi, kisaikolojia, kimwili na kiroho ambao amedai umekuwa tishio hapa nchini na kuleta madhara ya jamii kwa wananchi kukata tamaa ya maisha baada ya kukosa mahitaji yao muhimu kwa wakati

Akichangia mada hiyo Edith Nelson mwanafunzi wa Babati Day Sekondari alitaja madhara yatokanayo na ukatili huo kuwa ni pamoja na kuathirika kisaikolojia,vifo kutokana na ukeketaji,ulemavu wa kudumu,ongezeko la watoto wanaoishi mitaani,magonjwa ya zinaa yanayotokana na ubakaji na Ukimwi

Alisema hali hiyo imechangia jamii kuingia katika mfumo mbovu wa maisha ambao unaleta madhara makubwa na kuilazimu Serikali kufanya kazi ya ziada kukabiliana na vitendo vya kihalifu ambavyo ilikuwa kwao rahisi kukabiliana navyo kwa njia ya kuealimisha umma kuepukana navyo

“Tunashuhudia Serikali ikipambana na wahalifu wa aina mbalimbali wakiwemo vibaka,wauaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi Albino,majambazi,na kila aina ya uhalifu haya ni matoko ya ukatili uliokwisha fanyiwa watu hao na sasa wanalipiza visasi”alisema

Aina nyingene ni kushuka kwa kiwango cha elimu kwa wanafunzi mara wazazi wanapoachana, mmomonyoko wa maadili ndani ya familia, mimba zisizotarajiwa kusambaratika kwa familia na wazazi kulipa visasi kwa watoto wao kuwapa mateso mara wanapowazaa

Kwa upande wake Nenduvoto Wilson (mwanafunzi) wa Babati day Sekondari alitaja madhara mengine kuwa ni pamoja na kupungua kwa nguvu kazi ya Taifa kwa wahanga kupata vilema vya kudumu kama vile kukatwa viungo vya mwili hivyo kuwa tegemezi kwa jamii

Naye Nice Zacharia mwanafunzi wa Babati day aliitaka jamii kuacha kuwa na mtazamo hasi wa kuelimisha watoto kwa ubaguzi hasa wa kike kukosa fursa hizo adhimu kwa madai ni wakuolewa tu na sio kufanya kazi kama walivyo wa kiume

“Ubaguzi huu uko katika nyanja mbalimbali zikiwemo shuleni mtoto wa kike akitaka uongozi inatafsiriwa kuwa anataka kufanya kazi ya kiume ili hali kuna ushahidi unaoonyesha mafanikiwa makubwa katika kazi mbalimbali wafanyazo wanawake nchini”alisema



Maoni