KITETO YAMNYIMA PINDA USINGIZI


Kiteto yamnyima usingizi Pinda 

Na.Mohamed Hamad Manyara
Mauaji yanayoendelea kujitokeza kila mara kati ya wakulima na wafugaji wilayani Kiteto mkoani Manyara yamedaiwa kumnyika usingizi Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano Mizengo Kayanza Pinda

Hayo yameelezwa na Kanal Kininyang’ombe Nzoka Mkuu wa Wilaya ya Kiteto aliyeshika nafasi ya Martha Jaki Umbulla wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM 2014/2015 kuwa imetekelezwa kwa zaidi ya 75%

 “Wilaya ya Kiteto imekuwa na majina mengi, imeitwa Somalia na majina mengine ya maeneo yenye vita kutokana na mauaji yanayoendelea kujitokeza naomba uwepo wangu uchukuliwa kutaka kukomesha migogoro hii”

“Nitafanikiwa endapo nitapata ushirikiano wa kutosha kutoka kwenu ambao utaleta mahusiano mema kati ya wakulima na wafugaji kama jitihada zinavyoendelea kufanywa na mamlaka mbalimbali zikiwemo tume zilizoundwa na uongozi wa juu”alisema

Hata hivyo migogoro hiyo imetajwa kuwa na changamoto nyingi zikiwemo zile za ukabila,rushwana hata kutowajibika kwa baadhi ya viongozi katika nafasi zao huku wananchi wakiendelea kupoteza maisha

Katika kikao hicho cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM baadhi ya wajumbe walihoji kutokamilika kwa baadhi ya miradi huku kukiwa na  changamoto za ukosefu wa fedha Serikalini toka kwa baadhi ya viongozi

Akijibu hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri ya Wilaya Bosco Ndunguru aliwatoa wasiwasi wajumbe hao kuwa bado kuna muda wa kutosha kukamilisha miradi hiyo hadi mwezi wa wasaba ambao ndio unakamilika mwaka wa Serikali

Hata hivyo baadhi ya wananchi waliozungumzia miradi hiyo walisema bado kuna changamoto nyingi katika upatikanaji wa huduma za jamii zikiwemo maji afya na elimu kuwa Serikali ijipange katika kuondoa mapungufu hayo

Mwisho

Maoni