Mwenyekiti CHADEMA Monduli akanusha kuahamia CCM


Mwenyekiti CHADEMA Monduli akanusha kuahamia CCM

Na MOHAMMED SHAABAN MONDULI
MWENYEKITI wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA wilayani Monduli Japhet Sironga amekanusha uvumi wa kisiasa kuwa amehamia CCM wakati wa ziara ya katibu mkuu wa CCM Abrahaman Kinana akiwa mkoani Arusha

Hatua hiyo imefikiwa na mwenyekiti huyo baada ya wanachama wake kuendelea kumhoji juu ya uvumi huo ambao alidai kuwa sio kweli na anashangaa kusikia kuwa amehama chama tena kupitia  mikutano ya CCM

“Ninachofahamu kuna bwana mmoja aliyewahi kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Mch.Amani Silanga maarufu Ole Njakai ndiye aliyetangaza kujiunga na CCM baada ya kufukuzwa na CHADEMA na kuvuliwa nyazifa zake zote”alisema Sironga mwenyekiti wa CHADEMA Monduli

“Huyu bwana ifahamike kuwa alifukuzwa uanachama toka Nov 17 mwaka 2013 na kuvuliwa nyazifa zote ndani ya chama baada ya kuonekana kufanya hila za kutaka kukihujumu chama”alisisitiza Sironga

Baadhi ya nyazifa alizokuwa nazo ni pamoja na uenyekiti wa chama Wilaya na mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA Taifa ambazo alizipata kwa kuaminiwa na wanachama kushikilia

Bw. Sironga aliwataka wanachama hao kuepuka majungu na propaganda za kisiasa ambazo zinatapakazwa na wanaCCM kuwa Monduli hakuna CHADEMA wala wanachama akisisitiza kuwa chama kimeenea kata zote 20 za wilayani Monduli

Mwisho

Maoni