RC Manyara azindua mradi wa maji wa 134.1 mil


RC Manyara azindua mradi wa maji wa 134.1 mil

NA.MOHAMED HAMAD KITETO
MKUU wa Mkoa wa Manyara Dr Joel Bendera amezindua mradi wa maji wa kitongoji cha Kona kijiji cha Kijungu wilayani Kiteto mkoani Manyara ambao utanufaisha wakazi 3,078 wa kata ya Kijungu ambao walitaabika na huduma hiyo

Mradi huyo wenye thamani ya 134,107,000 umejengwa chini ya mpango wa maji vijijini WSDP kwa ushirikiana wa Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia kwa lengo la kukabiliana na uhaba wa maji vijijini

Ikisemwa risala kwa mgeni rasmi ilieleza mradi huo umehusisha ujenzi wa nyumba moja ya mashine,mbauti,tanki la ujazo wa mita 50,ujenzi wa nyumba moja ya mlinzi,vituo 3 vya kuchotea maji,ununuzi na ufungaji wa genereta moja ya umeme na pampu na kutandaza mabomba

Kwa mujibu wa Jemsi Kionaumela Mhandisi wa maji wilaya alisema mradi huo  umekamilika na utawanufaisha wananchi wa vijiji zaidi ya vitatu na vitongoji vyake wapatao 3078 katika kata ya Kijungu

“Mheshimiwa mkuu wa mkoa mradi huu umekamilika una uwezo mkubwa wa kuwaondolea adha wananchi wa maeneo haya ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitaabika na tatizo la maji na kushindwa kufanya shuhuli zingine za maendeleo”alisema Eng.Jemshi Kionaumela

Kwa upande wa wananchi wa kitongoji hicho cha kona walimweleza mkuu huyo wa mkoa kuwa ndoa zao ziliyumba kutokana na kutoaminiana kwa wanadoa kutokana na wanawake kutumia muda mwingi kusaka maji

“Tulikuwa tukipigwa na waume zetu wakati mwingine tunapochelewa kurudi nyumbani na hii sio kutokana na michepuko bali ni kwa kuchelewa kupata maji sambamba na wivu wa mapenzi kwa waume zetu” alisema mmoja wa wanawake kijijini hapo

Akihutubia wananchi hao Dr Joel Bendera aliwataka wananchi hao kulinda mradi huo wa maji ambao ni adhimu akisema kuna hulka za watu ambao hata Mungu anawajua kuwa wanatabia ya uchokonozi kama akina tomaso

“Hapa kuna akina thomaso hawakosekani,nemeambiwa mradi huu ulianza kuhujumiwa sasa naagiza mtu yoyote atakaye hujumu mradi sheria kali zitachukuliwa dhidi yake kwani hatuwezi kuwavumilia watu wa aina hii”alisema

Awali katika kile kilichodaiwa kushangaza viongozi na wananchi wengi mtu ambaye hajafahamika siku chache kabla ya uzinduzi aliweka chumvi kwenye mashine hiyo ya maji ili isifanye kazi jambo ambalo liliibua hisia tofauti kwa wakazi

Mwisho

Maoni