VIONGOZI VIHIYO CHANZO CHA MATATIZO NCHINI


Picha na Mohamed Hamad Manyara

Viongozi vihiyo chanzo cha matatizo Nchini.

Na Mohamed Hamad Manyara.
Usaliti wa baadhi ya viongozi wa Serikali na vyama vya Siasa hapa nchini wa kutotenda majukumu yao ipasavyo ndani ya jamii umetajwa kuwa ni moja ya matatizo yanayolilikumba Taifa katika kutaka kufikia malengo yake tarajiwa.

Hayo yameelezwa na Wakili Mjengi Lissu wa Kituo cha Utawala wa Sheria na mazingira (CELG) wakati akiwasilisha mada ya vyombo vya usimamizi wa sheri na haki za Binadamu kwa wasaidizi wa kisheria 25 kutoka mashirika yasiyokuwa ya kiserikali Wilayani Kiteto.

“Umefika wakati baadhi ya viongozi wa Serikali wanakuwa sio wazalendo,waadilifu katika nyazifa zao walizonazo huku wakionekana kuwasaliti wananchi kwa kushindwa kufanya maamuzi yenye tija kwa maslahi yao binafsi”.

Alisema haya yatakwisha endapo jamii itaendelea kuelimika na kujua wajibu wao na kuhoji na hata kukataa kile kinacholazimishwa na watawana wao ambacho kinaaminika kuwa hakina tija na hakiwezi kuwa na maslahi na Taifa kwa baadaye.

Alitolea mfani wa Jinsi deni la Taifa linavyozidi kukuwa akisema kuna baadhi ya viongozi wamelewa madaraa wakisema kuaminika kwa nchi ya Tanzania kwa wafadhili imekuwa fursa ya kuendelea kukopa bila kufikiri namna ya kulilipa deni hilo.

Kwa upande wake Mashaka Saidi Fundi (mjumbe) alisema  anashangazwa na mfumo uliopo Tanzania kuwa watu wote wanalalamika wakiwemo viongozi vyama na Serikali na hata wasomi badala ya kutafuta ufumbuzi wa kutatua matatizo.

“Nilimsikia Katibu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana akiwa Dodoma analalamikia baadhi ya Viongozi wa Serikali wanaowajumu wananchi kwa Nyanja mbalimbali akiwataka wawajibike akidai huko ni kukwepa majukumu yake kuwa alipaswa kuchukua hatua  dhidi ya viongozi hao”.

Nae Hassani Konki akiongea kwa jazba alisema utaratibu huu utazaa Taifa la watu wasio waadilifu wenye kupinga Serikali yao iliyopo madarakani huku Viongozi wao wakitumia nguvu kubwa kuzuia na hata kuwaua.

Alidai katika maeneo mengi kumekuwepo na vurugu za uchaguzi zinazojitokeza kwa kutowaamini wasimamizi kwa madai ya kulindana jambo ambalo limeleta madhara makubwa kwa wananchi yakiwemo maafa.

Katika mafunzo hayo washiriki hao wamelaani vitendo vunavyo jitokeza vya mauaji kati ya wakulima na wafugaji kila mara huku Serikali ikidaiwa kushindwa kuyadhibiti kwa kile kilichodaiwa kuwepo kwa Rushwa na ukabila.

Mwisho

Maoni