KITETO NA MKAKATI WA KUBORESHA ELIMU


Kiteto na mkakati wa kuboresha elimu.

Na Mohamed Hamad Manyara
Sekta ya elimu ni taa ya maendeleo,nasema hivi nikimaanisha hakuna Taifa lililoendelea bila elimu,  mataifa hayo yalifanikiwa kutokana na kuweka elimu kuwa kipao mbele chao katika bajeti za maendeleo

Kwa miaka saba iliyopita wilaya ya Kiteto na mkoa wa Manyara kwa ujumla elimu haikuwa ikipewa nafasi ya kutosha, hivyo wanafunzi walionekana shuleni kama moja ya eneo la kusogeza umri ili waweze kuolewa ama kuoa

Na moja ya sababu zilizotajwa ni uhaba wa samani na thamani,waalimu kuwa wachache,mazingira duni ya kujifunzia na kufundishia,malalamiko ya waalimu bila kutafutiwa ufumbuzi pamoja na uhaba wa nyumba za walimu

Kutokana na changamoto hizo kiwango cha elimu Kiteto na Manyara kwa ujumla kilishuka katika miaka hiyo siku hadi siku huku wananchi wakiendelea kukosa haki ya msingi kupata elimu sahihi ambayo ilipaswa kutolewa na Serikali

Wilaya ya Kiteto kwa miaka ya 2010 iliendelea kushika nafasi mwisho kati ya wilaya sita za mkoa wa Manyara zikiwemo Babati mjini, Babati vijijini, Mbulu,Hanang, Simanjiro na Kiteto yenyewe

Katika kukabiliana na changamoto hizo ilisaidia wilaya ya Kiteto na mkoa kwa ujumla kupanda kielimu jitihada kubwa zilifanywa zikiwemo zile za kuhakikisha wanapunguza malalamiko ya waalimu pamoja na kuboresha sehemu za kujifunzia na kufundishia

Afisa elimu wa wilaya ya Kiteto Emmanuel Mwagala katika jitihada za kukuza elimu wilayani Kiteto alieleza kuwa wilaya imepata mafanikio makubwa yakiwemo kutoka katika nafasi ya mwisho hadi ya pili kimkoa

Alisema kwa sasa Kiteto inashikilia nafasi ya pili kimkoa kwa miaka miwili mfululizo kutokana na mikakati mbalimbali ikiwemo ya wanafunzi kula shuleni tofauti na hapo awali walipokuwa wanalazimika kushinda na njaa wakiwa shule hadi watakaporudi nyumbani

Mwingine ni waliongeza idadi ya waalimu ambapo awali shule moja ilikuwa na mwalimu mmoja ama wawili huku ikiwa na idadi ya wanafunzi zaidi ya mia tano kutokana na Serikali kushindwa kuajiri kulingana na uhitaji wa waalimu katika shule nyingi hapa nchini

Motisha nayo ilisaidia kwa kiwango kikubwa kwa waalimu na hata wanafunzi waliokuwa wanafanya vizuri ambapo walileta ushindani wa hali ya juu jambo lililofanya kiwango hicho cha elimu kupanda alisema Mwagala

Hata hivyo Afisa huyo wa elimu katika mahojiano maalumu alisema jumla ya wanafunzi bora 17  wakiume 9 na wakike 8 kati ya 20 waliofanya vizuri mkoani Manyara walitoka Kiteto

“Niseme tu hata mwanafunzi bora kimkoa wametoka wilaya ya Kiteto tena katika shule ya msingi Boma, huku shule tatu za kiteto zikiendelea kuchuana ikiwemo ya Boma, Lalakir, na Namelock”alisema Mwagala

Alisema kuwa mkoa ulihamasika nao na kupongeza wilaya ambapo walitoa kikombe cha dhahabu huku Taifa nao wakihamasika na kutoa medani moja ya dhahabu pamoja na ya fedha moja

Shule mbili zilipewa mil 3 kila moja kwa jitihada kubwa za katika kuchupa kutoka nafasi za nyuma hadi kuingia katika alama zuri ambapo shule hizo ni  partimbo na ilera na kwamba zilifanikiwa kupata kiasi cha mil 3 kila moja kama moja ya motisha

Kuhusu changamoto za uhaba wa nyumba za waalimu madarasa mapunjo ya waalimu  pamoja na samani na thamani Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Bosco Ndunguru aliyema Serikali imejipanga kukabiliana na tatizo hilo

Alisema suala la madawati kuna fursa Kiteto ya kuwa na msitu wa Suledo ambao umeanza kuvunwa mbao utatumika kama fursa ya kuhakikisha kila shule inapata madawati ya kutosha ili kupunguza adha ya wanafunzi kukaa chini

Kwa upande wao wadau wa maendeleo wamekosoa jitihada zinazofanywa na wilaya kuendeleza jitihada hizo wakisema bado kuna malalamiko ya waalimu ambayo hayakashuhulikiwa ipasavyo hivyo kuna uwezekana wa kushuka tena elimu

“Ninachojua bado hadi leo waalimu wanatishiwa amani mahali pa kazi na baadhi ya wananchi wa misingi ya kufuatilia wanafunzi watoro Serikali haijajipanga sawasawa kwani ni hatari”alisema Abasi Famao mdau wa elimu

Kwa upande wa chama cha waalimu wilayani Kiteto wamedai iko haja ya kuwepo kwa mfumo mzuri wa kushuhulikia matatizo ya waalimu Serikalini tofauti na ilivyo sasa kuwa kada ya waalimu inaonekana kama haina umuhimu ndani ya jamii

Utakuna mwalimu anakamatwa akifundisha eti kwasababu tu hajalipa mchango wa maabara, hivi hakuna njia nyingine mbadala ya kupata fedha hiyo mpaka umkamate mwalimu wakati akifundisha alihoji Ghambos Sule mwenyekiti wa chama cha walaalimu mkoani Manyara

INAENDELEA…

Maoni